2013-11-20 15:02:26

Mkutano juu ya Mabadiliko ya tabia nchi: viongozi fikirieni leo na kesho


Jumatatu19 Novemba 2013, Mkutano wa Kimataifa juu ya mabadiliko ya tabia nchi (COP 19) ulioanza wiki iliyopita na vikao vya tume tendaji, , ulifunguliwa rasmi mjini Warsaw Poland na kuhudhiriwa na wakuu wa nchi kadhaa, wajumbe wawakilishi wa makampuni na mashirika na viwanda, vyombo vya habari na taasisi za utafiti.
Lengo la Mkutano huu wa wiki mbili, unaokamilika 22 Novemba 2013, ni kukutanisha watalaam toka mataifa mbalimbali, ili washrikisha utajiri wa ufahamu na uzoefu katika masuala yanayo gandamiza uchumi, na uwepo wa mabadiliko katika tabia nchi. Na pia kujadili dharura zinazo tajwa na jumuiya ya kisayansi , katika hoja ya binadamu kuwa makini na utendaji wake.
Mkutano huu ni ufuatiliaji wa majadiliano yanayo lenga katika kukamilika kwa Malengo ya mwaka 2015, na makubaliano ya kimataifa yanayo lenga malengo ya COP21, yatakayo fanyika mjini Paris , lkama ilivyo kubalika mwaka jana katika mkutnao wa COP18 Doha, Qatar.
Majadiliano ya mjini Paris, yanatazamiwa kutengeneza utekelezaji hadi 2020 wakati ambapo wengi wataweza kushuhudia maana ya lengo la kupunguza ongezeko la joto duniani kwa nyuzi joto mbili nje, ambalo limeshndikana kufikiwa.

Tume ya Umoja wa Mataifa juu ya Mabadiliko ya Hewa, UNFCCCC, katika tamko lake la Jumatatu , wakati wa kuanza rasmi mkutano wa COP 19 mjini Warsaw, limetoa wito kwa serikali ya kuunganisha utendaji wa nguvu dhidi ya mabadiliko ya hali ya hewa katika ngazi zote za utendaji wa serikali na jamii na kufanya maendeleo halisi, kuelekea mafanikio katika mkataba wa Kimataifa wa mabadiliko ya tabia nchi, kwa mwaka 2015.

Rais mpya aliyechaguliwa na Mkutano wa Wanachama (COP 19/CMP9 ), Mheshimiwa Marcin Korolec, Waziri wa Mazingira Poland, katika hotuba yake ya ufunguzi, ameeleza kuwa, mabadiliko ya tabia nchi ni tatizo la kimataifa, ambalo ni lazima kulifanya lipige “about turn”. Ni tatizo kama hatuwezi kuratibu vitendo vyetu, na lazima kutenda kwa ushirikiano. Utendaji wa nchi moja au kikundi kimoja kimoja hakuwezi kusitisha tatizo. Na ni sisi binadamu tunaotakiwa kuungana na kutenda kwa mshikamano mmoja, ili kulinda vizazi vya sasa na ya baadaye.









All the contents on this site are copyrighted ©.