2013-11-19 07:58:35

Maisha ya Kikristo yanarutubishwa kwa Sakramenti, Neno la Mungu na matendo ya huruma!


Askofu msaidizi Eusebius Nzigilwa, Mwenyekiti wa Idara ya Katekesi, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mahojiano na Radio Vatican anabainisha umuhimu wa waamini kuifahamu kwa kina Katekisimu Mpya ya Kanisa Katoliki, muhtasari wa Imani, Sakramenti za Kanisa, Maisha Adili na Sala inayomwilishwa katika matendo. RealAudioMP3

Imani thabiti ni chachu inayomwezesha mwamini kuyatakatifuza malimwengu kwa njia ya ushuhuda wa imani yake kwa Kristo na Kanisa lake. Maisha ya Mkristo yanapata mwanzo wake kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo, mlango wa imani unaomwezesha mwamini kupata Sakramenti nyingine za Kanisa. Maisha ya mwamini kiroho hayana budi kurutubishwa kwa Sakramenti, Neno la Mungu na matendo ya huruma.







All the contents on this site are copyrighted ©.