2013-11-19 10:01:18

Kuna haja ya kulinda na kudumisha heshima ya kazi na utu wa wafanyakazi!


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu tarehe 18 Novemba 2013 amekutana na kuzungumza na Bwana Guy Ryder, mkurugenzi mkuu wa Shirika la Kazi Duniani, ILO, ambaye amesema kwamba, Kanisa na Shirika lake linakazia umuhimu wa kulinda na kudumisha heshima ya kazi na utu wa wafanyakazi, hasa wale wanaotekeleza majukumu yao katika mazingira hatarishi.

Viongozi hawa wawili wanasikitishwa sana na ongezeko la biashara haramu ya binadamu inayoendelea kuwatumbukiza wanawake na wasichana katika utumwa mamboleo. Kazi yenye hadhi na utu wa binadamu ni kati ya mambo msingi yanayotarajiwa kutekelezwa na Jumuiya ya Kimataifa baada ya kukamilika kwa Malengo ya Maendeleo ya Millenia kwa Mwaka 2015.

Shirika la Kazi Duniani, linashirikiana kwa karibu zaidi na Taasisi za Kanisa Katoliki na kwa namna ya pekee na Baraza la Kipapa la haki na amani katika mchakato wa kuhakikisha kwamba, haki jamii inazingatiwa na wengi. Bwana Ryder amekutana na kuzungumza pia na viongozi wa Serikali ya Italia pamoja na vyama vya kiraia







All the contents on this site are copyrighted ©.