Rwanda na Msumbiji ni nchi pekee za Jumuiya ya Madola ambazo hazikutawaliwa na Mwingireza,
lakini zinashiriki katika mkutano wa Wakuu wa Jumuiya hii unaoendelea mjini Colombo,
Sri Lanka. Jumla ya wakuu wa nchi 54 wanachama wa Jumuiya ya Madola wanashiriki, ingawa
kuna kinzani kati ya India na Canada wanaoitaka Sri Lanka kufanya uchunguzi wa kina
kuhusu vita na mauaji yaliyojitokeza nchini humo kunako mwaka 2009.
Msimamo
kama huu pia umetolewa na Uingereza kwa kuituhumu Sri Lanka kufanya mauaji ya kinyama
dhidi ya wananchi wa Tamil, shutuma ambazo zimetupiliwa mbali na Rais Mahinda Rajapakse
wa Sri Lanka.