2013-11-14 10:42:50

Majadiliano ya kidini yanalenga kuwasaidia watu kumfahamu Mungu


Kardinali Gianfranco Ravasi, Rais wa Baraza la Kipapa la Utamaduni kuanzia tarehe 14 hadi 16 Novemba 2013 yuko nchini Jamhuri ya wananchi wa Cheki kama sehemu ya mwendelezo wa majadiliano ya kidini na waamini wasiomwamini Mungu. Akiwa nchini humo Kardinali Ravasi amepangiwa ratiba ya kukutana na kuzungumza na viongozi wa Serikali, wanadiplomasia, wasomi na wanazuoni pamoja na wawakilishi kutoka katika dini na madhehebu mbali mbali ya Kikristo n chini humo.

Kardinali Ravasi, Ijumaa tarehe 15 Novemba 2013 anatarajiwa kufanya majadiliano na wasomi mbali mbali kuhusiana na mambo ya imani na malimwengu katika nyakati hizi. Hizi ni juhudi zilizoanzishwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita, aliyetamani kuliona Kanisa la Kristo likiendeleza majadiliano ya kidini na wale wasiomwamini bado Mungu, ingawa wana kiu na hamu ya kusikia kweli za Kimungu katika hija ya maisha yao!







All the contents on this site are copyrighted ©.