Balozi mpya wa Vatican nchini Ujerumani awasili tayari kuanza utume wake!
Askofu mkuu Nikola Etrovic, Balozi mpya wa Vatican nchini Ujerumani aliyeteuliwa hivi
karibuni na Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 14 Novemba 2013 amewasili nchini
Ujerumani tayari kuanza utume wake, kama Mwakilishi wa Vatican, baada ya kulitumikia
Kanisa kama Katibu mkuu wa Sinodi ya Maaskofu Katoliki mjini Vatican.
Uwanja
wa ndege wa Berlin- Tegel, Askofu mkuu Etrovic amepokelewa na viongozi mbali mbali
wa Kanisa na Serikali kutoka Ujerumani, wakiongozwa na Kardinali Rainer Maria Woelk.