2013-11-13 15:10:23

Maungamo ni ubatizo wa pili katika utakaso wa dhambi


Jumatano hii , Papa Francisko amewataka waumini wote kujenga tabia ya kuugama dhambi kwa unyenyekevu na kuomba msamaha kwa Mungu , kila mara wanapotenda dhambi, ili kupata neema za utulivu wa moyo na furaha.
Wito huu ni sehemu ya ujumbe wa Papa kwa waumini, ambao ameutoa kupitia Katekesi yake ya Jumatano, kwa mahujaji na wageni , waliokusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Alisema kama ilivyo katika ubatizo ambamo dhambi ya asili na dhambi zingine hutakatifushwa, pia Sakramenti ya Kitubio, hufungua mlango wa maisha mapya ya kiroho , wakati huruma ya Mungu inapoingia ndani ya maisha yetu.
Papa alieleza haya akiendelea kutafakari juu ya sala ya Nasadiki, ambamo leo amegeukia Sakramenti ya Ubatizo, akisema, kila Jumapili wakati wa kukiri imani yetu , tunasali: Nakiri katika ubatizo mmoja kwa msamaha wa dhambi.
Papa aliyatazama maneno hayo kwa kina na mara kutoa mwaliko kwa waliokuwa wakisikiliza, kutafakari pamoja nae , neno hadi neno lililoandikwa katika aya hii. Alianza na neno ninakiri, akisema, ni neno kuu linaloonesha umuhimu wa Ubatizo na kuthibitisha utambulisho cha mbatizwa kuwa mtoto wa Mungu. Katika Sakramenti , imani yetu pia inahusishwa na maondoleo la dhambi. Tunapo ungama dhambi zetu , pia tunafanywa upya kiroho na kuimarisha utambulisho wa ubatizo wetu. Na hivyo basi , ubatizo , inakuwa ni mahali pa kuuanza mwendo wa safari ndefu ya maisha yote ya uongofu endelevu, yanayolishwa na Sakramenti ya Kitubio .
Na maneno Ubatizo Mmoja – ambamo neno ubatizo linamaanisha kuzamisha, kwa njia ya Sakramenti hii, muumini huizamisha roho yake katika kifo cha Yesu Kristo, na kufufuka naye kama kiumbe kipya. Akiwa amefanywa upya na maji na Roho Mtakatifu , humlikiwa na mwanga wa neema ambayo hufukuza uvuli wa dhambi.
Papa Francisko aliendelea kueleza kwamba, kwa maneno kwa msahama wa dhambi,maneno haya yanaonyesha kwamba, Ubatizo huondoa dhambi ya asili na dhambi ya nyingine binafsi. Na hivyo , kwa ubatizo, mlango kwa maisha mapya hufunguliwa na huruma ya Mungu huingia katika maisha yetu. Lakini , Papa alionya kwamba udhaifu wa binadamu hubaki palepale. Ndiyo maana kanisa linatufundisha kuungama dhambi zetu kwa unyenyekevu mara kwa mara , kwa sababu tu katika msamaha,tupewana kupokea neema ya kuifanya mioyo yetu yenye kuhangaika daima, kupata amani na furaha.








All the contents on this site are copyrighted ©.