2013-11-13 15:37:03

Maaskofu wa Ufilipino watoa wito wa Novena kwa wahanga wa Kibunga.



Maaskofu Katoliki wa Ufilipino, wametoa wito wa Novena, sala na fadhila, kwa waathirika na familia zilizopigwa vikali na maafa ya kimbunga kilichopita hivi karibuni na kuua mamia ya watu na kuharibu mali nyingi, zikiwemo nyumba.

Mosinyori Pedro Quitorio , Mkurugenzi wa vyombo vya habari katika Baraza la Maaskofu Katoliki ya Philippines , alisema fedha zitakazo tolewa wakati wa kipindi cha Novena , iliyoanza Jumanne 12 na itaendelea hadi Novemba 19, zitaelekezwa katika Majimbo yaliyo athirika zaidi na kibunga kupitia tawi la Caritas Ufilipino. Na alitaja majimbo yaliyopigwa zaidi kuwa ni Jimbo la Borongan na Jimbo Kuu la Palo .

Katika jimbo la Borongan , ambako kibunga kilianzia , kimeharibu pia kanisa kongwe lililo tajwa na UNESCO, kuwa urithi wa duniani, ambalo liliwaka moto na kuharibiwa karibia kwa 85-95 pamoja na nyumba zilizokuwa katika parokia hiyo pia zimeharibiwa, ingawa kwa jinsi ilivyofanyika, kunaleta utata wa kujiuliza maswali mengi juu ya hilo.
Katika mkoa wa Palo , ambako kuna mji wa Tacloban , watu wengi wamefariki duniani. Askofu Quitorio anasema , ingawa miundombinu na kanisa mengi yameharibiwa , ikiwa pamoja na Makao Makuu ya Palo na kaburi muhimu ya Mtakatifu Nino. Kipaumbele kwa wakati huu ni ksaudia watu kuishi na sio majengo.

Na akizungumzia haja ya kupeleka viongozi zaidi wa kiroho katika eneo hilo anasema, ni vyema kufanya hivyo. Lakini kwa wakati huu kinachohitajika zaidi ni kukusanya fedha kwa ajili ya upatikanaji wa msaada wa kwa ajili ya chakula , maji na dawa.

Licha ya hivyo , kw awakati huu katika badhi ya miji iliyokubwa hakuna tena utaratibu wa kiserikali, watu wanapora vitu , wanaingia k tiak mafuka wakitafuta chakula chao. Hakuna sheria na utaratibu hivi sasa. Hii ni wasiwasi wetu wa kwanza. Serikali haijaweza kusitisha uasi huu . Kanisa linatumaini , serikali itawweza kurejesha amani na utulivu haraka iwezekanavyo, na hasa katika tararibu za msaada unaotolewa kuwafikia wahitaji wote bila usumbufu mkubwa.










All the contents on this site are copyrighted ©.