Onesheni moyo wa sala na ukarimu kwa wananchi wa Ufilippini na Vietnam waliofikwa
na maafa!
Baba Mtakatifu Francisko anaendelea kufuatilia kwa karibu mateso na mahangaiko ya
wananchi wa Ufilippini pamoja na Vietnam waliokumbwa na kimbunga cha Haiyan, kinachoendelea
kusababisha maafa makubwa kwa wananchi wengi Barani Asia.
Baba Mtakatifu katika
ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, anawaalika kwa namna ya pekee kuwakumbuka
katika sala na matendo ya huruma wananchi wa Ufilippini na Vietnam, ambao kwa sasa
wanakabiliana na hali ngumu ya maisha baada ya maafa yaliyosababishwa na kimbunga
cha Haiyan.