2013-11-12 15:35:54

Kwa Wakristu ni muhimu kuheshimu tofauti za kilitujia zilizopo- AskofuMkuu Martin aeleza.


(Vatican Radio) Kwa jinsi gani nguvu na uhai wa yatokanayo na mkutano wa 10 wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni, vinaweza kuleta msukumo mpya katika harakati za kiekumeni ? Na kwa jinsi gani Wakristo wa madhehebu mbalimbali wanaweza kugundua upya asili ya mizizi yao ya kiroho kwa pamoja? Na jinsi viongozi Katoliki wanalenga kutekeleza malengo ya Mkutano huu wa 10 wa WCC ndani ya maisha ya Makanisa yao ?

Ni maswali yaliyotolewa na Philippa Hitchen kwa Askofu Mkuu wa Dublin, Diarmuid Martin, mjumbe Katoliki katika mkutano wa 10 wa WCC, na Mratibu mwenza aliyemaliza muda wake wa kuwa mjumbe katika utume wa pamoja katika Kazi za Kanisa Katoliki kwenye Baraza la Makanisa Ulimwenguni.
Askofu Mkuu Martin alijibu maswali na maeelzo kwamba, kati ya yote kwake yeye maazimio yaliyotolewa juu ya vijana ,yanayo himiza kutunza mizizi ya kiroho ya kiekumene inaonyesha kwamba, kwa kadri Wakristu wanavyo elewa utendaji wa kufanana wa watakatifu, katika maisha yao ya kawaida ndivyo twanavyo zidi kukaribiana katika misingi ya kiekumeni.
Na kwa jinsi hiyo, kwa kutazama Maadiko ya Kiliturujia , nyimbo na maandiko ya Kikristo, kabla ya mgawanyiko wa Wakristu, mna onekana vile vinavyo waunganisha pamoja Wakristu , ingawa kwa kwa bahati mbaya , ameonya, muda wa kutosha hautolewa katika kuyatazama hayo kwa makini zaidi.
Askofu Mkuu Diarmuid anasema baada ya mkutano huu, ujumbe anaopeleka nyumbani kama Askofu wa jimbo , ni kuhakikisha uzoefu alioupata katika mkutano huu, anaushirikisha pia kwa jimbo lake, kwenye maisha ya siku hadi siku ya Kikristo Jimboni mwake na pia katika nchi nyingine ....
Anaendelea kueleza kwamba, uzoefu wa wa Mkutano huu kwenye ngazi ya kibinadamu na kiroho, ni maajabu.Umekuwa ni kati ya mikutano michache sana ya aina hii iliyowahi kufanyika duniani kwa Wakristu kuuishi mchanganyiko huu kwa maelewano ya kujiona wao ni kundi moja linaloongozwa na Mchungaji mmoja Kristu. Na hivyo anaona kwamba, umoja Wakristu haupaswi kuishia katika umoja na mshikamano wa kufanana katika kila jambo, lakini hatima yake inapaswa kuhakikisha utofauti wa utendaji wa kiliturujia unaheshimiwa katika maisha ya Kanisa zima...

Na kwamba, kuna nguvu fulani katika Mkutano huu, mengi yakitokana na ukweli kwamba, vijana wameshirikishwa katika mkutano huu. Na hivyo amebaki akijuìiuliza kama inafaa pia, kwa mfano katika mkutano ya Sinodi ya Maaskofu Katoliki , kuwa na uwezekano wa kuwa na mchanganyijko wa aina hii , kuishirikisha pia furaha hii ya vijana , na hata uhuru wa kuwa wachokozi tu, katika baadhi ya changamoto zinazo pambanisha Kanisa . Kwake yeye anadhani pia hilo ni muhimu.









All the contents on this site are copyrighted ©.