2013-11-11 16:42:09

Tanzia: Kardinali Domenico Bartolucci amefariki dunia


Tunasikitika kutangaza kifo cha Kardinali Domenico Bartollucci kilichotokea mapema Asubuhi Jumatatu hii 11. 11 2013. Kardinali amefikwa na mauti akiwa na umri wa miaka 96.
Kwa kifo chake, Idadi ya Makardinali imebaki 200, ambamo kati yao wenye haki ya kikatiba kupiga kura ni 109 na wasiokuwa na haki ya kupiga kura ni 91.
Marehemu kwa muda wa miaka mingi alikuwa ni Mkurugenzi wa Muziki Mtakatifu wa Kipapa katika kanisa ldo la Sistini ndani ya Vatican. Alifanywa kuwa Kardinali na Papa Benedikto XV1, wakati wa kikao cha Makardinali "Consistory" tarehe 20 Novemba 2010.
Mara baada ya taarifa ya kifo kumfikia Papa Francisko , mara aliandika na kutuma salaam zake za rambirambi kwa ndugu wa Marehemu Sandro na Stefano Bartolucci , na kwa jumuiya ya Jimbo la Fiorentina pamoja na wote waliouguwa kwa namna moja au nyingine na katika maombolezo haya.
Papa ametaja sifa za Marehemu kwamba alikuwa ni mtunzi maarufu na mwanamuziki aliyeyatolea maisha yake yote kwa ajili ya Muziki Mtakatifu, akionyesha utahabiti wa imani yake kwa Kristu. Papa ametoa shukrani kwa matunda yake kama Mkurugenzi wa Sistine Chapel, na hekima zake, katika upigaji wa muziki wa kumsifu Mungu. Papa ameeleza na kusali kwa maombezi ya Bikira Maria, kusmpokea mtumishi huyu wa Mungu katika makao ya milele.








All the contents on this site are copyrighted ©.