2013-11-09 11:54:09

Zimbabwe yawaambia wananchi wa Msumbiji, kupatana vinginevyo, watakiona cha moto!


Mgogoro wa kivita kati ya Serikali ya Msumbiji na Chama cha Upinzani za RENAMO umeanza kuchukua sura mpya kwa Zimbabwe kuzitaka pande zinazohusika, kutafuta suluhu ya haraka, vinginevyo, itauvalia njuga mgogoro huu na kutuma vikosi vyake vya kijeshi kupambana na waasi.

Zimbabwe inahofia ikiwa kama vita ya wenyewe kwa wenyewe itafumuka tena nchini Msumbiji, uchumi wake utazorota kwa kiasi kikubwa kwani inategemea kwa kiasi kikubwa Bandari ya Beira kwa ajili ya kusafirishia mizigo yake. Licha ya ukweli huu, wachunguzi wa masuala ya kijeshi wanasema kwamba, hii ni kejeli ya Zimbabwe tu, kwani haina uwezo wala jeuri ya kupeleka vikosi vyake nchini Msumbiji kutokana na kuendelea kukabiliana na hali ngumu ya uchumi.

Kunako mwaka 2003 Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC ilipitisha Azimio kwamba, inaweza kuingilia kati kwa kutuma majeshi, ikiwa kama siasa na demokrasia ya nchi mwanachama iko hatarini. Nje ya agizo la SADC, Zimbabwe, itakuwa inaingilia masuala ya ndani ya Msumbiji.







All the contents on this site are copyrighted ©.