Papa aguswa na mahangaiko ya wananchi wa Ufilippini
Baba Mtakatifu Francisko amepokea kwa masikitiko na majonzi makuu taarifa za mahangaiko
ya wananchi wengi wa Ufilippini kutokana na kukumbwa na kimbunga ambacho kimesababisha
maafa makubwa kwa watu na mali zao.
Baba Mtakatifu anawaalika waamini na watu
wote wenye mapenzi mema kujiunga naye kwa ajili ya kuwaombea waathirika wa kimbunga
hiki nchini Ufilippini.