2013-11-08 07:59:45

Serikali ya Chad na Vatican watiliana sahihi mkataba wa ushirikiano kwa ajili ya ujenzi wa Jamii inayosimikwa katika misingi ya haki na amani


Vatican na Serikali ya Chad, tarehe 6 Novemba 2013 wametiliana sahihi mkataba unaoliwezesha Kanisa nchini Chad kutambulika kisheria. Ujumbe wa Vatican katika makubaliano haya umeongozwa na Askofu mkuu Jude Thaddeus Okolo, Balozi wa Vatican nchini Chad na Bwana Moussa Mahamat Dabo, Katibu mkuu, Wizara ya Mambo ya nchi za nje na ushirikiano na utengamano wa Afrika amewakilisha serikali ya Chad.

Mkataba huu umegawanyika katika ibara 18 na utaanza kufanya kazi pale tu pande hizi mbili zitakaporidhia. Vyeti vinavyotolewa na taasisi za elimu nchini Chad vitaweza kutambulika na Serikali na kwamba, Kanisa na Serikali vinapenda kushirikiana kwa dhati kwa ajili ya kulinda na kutetea utu na heshima ya binadamu sanjari na ujenzi wa Jamii inayosimikwa katika misingi ya haki na amani.







All the contents on this site are copyrighted ©.