Heri za Mlimani kuongoza Maadhimisho ya Siku za Vijana Duniani 2014- 2016
Baba Mtakatifu Francisko amechagua tema zitakazoongoza Maadhimisho ya Siku ya za Vijana
Duniani kwa kipindi cha Miaka mitatu, kama sehemu ya maandalizi ya Siku ya Vijana
Duniani itakayofanyika mjini Cracovia, Poland, kunako Mwaka 2016. Mada zilizochaguliwa
na Baba Mtakatifu ni kutoka katika Heri za Mlimani, ambazo kimsingi ni Muhtasari wa
Mafundisho makuu ya Kristo.
Siku ya 29 ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2014 itaongozwa
na kauli mbiu: "Heri maskini wa roho, maana ufalme wa mbinguni ni wao. Mt. 5:3.
Siku
ya 30 ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2015 itaongozwa na kauli mbiu "Heri wenye moyo safi,
maana hao watamwona Mungu.
Siku ya 31 ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2016 itakayofanyika
Jimbo kuu la Cracovia, Poland, itasindikizwa na mada "Heri wenye rehema maana hao
watapata rehema." Mt. 5:7.
Itakumbukwa kwamba, Baba Mtakatifu Francisko alipokutana
na bahari ya vijana wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013
mjini Rio de Janeiro, nchini Brazil, aliwaalika vijana kufanya tafakari ya kina kuhusu
heri za Mlimani ili hatimaye waweze kuzimwilisha katika uhalisia wa maisha yao.
Hii
ni kutokana na ukweli kwamba, Heri za Mlimani ni muhtasari wa mafundisho makuu ya
Kristo na ni kanuni na mwongozo wa maisha ya kiroho!.