Dr. Mvungi yuko Afrika ya Kusini kwa matibabu zaidi!
Tume ya Mabadiliko ya Katiba inapenda kuwafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake Dr.
Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI)
amesafirishwa Alhamisi, Novemba 7, 2013) saa 5:45 asubuhi kwenda nchini Afrika Kusini
kwa uchunguzi na matibabu zaidi. Akiwa nchini Afrika Kusini, Dr. Mvungi atapata matibabu
katika Hospital ya Milpark iliyopo Jijini Johannesburg.
Itakumbukwa kuwa Dr.
Mvungi alivamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam
na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3,
2013. Tukio hilo la uvamizi linaendelea kuchunguzwa na vyombo vya ulinzi na usalama
nchini.
Tangu siku alipojeruhiwa, Dr. Mvungi alikuwa akipata matibabu katika
Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI). Hata hivyo, Madaktari waliokuwa wakimtibu MOI,
walishauri afanyiwe uchunguzi na matibabu zaidi. Dr. Mvungi ameondoka na ndege ya
kukodi ya Shirika la Ndege la Flightlink na ameambatana na Dr. Mugisha Clement Mazoko
kutoka MOI; Muuguzi Bi. Juliana Moshi; na mtoto wa kaka yake Bw. Deogratias Mwarabu.
Serikali inagharamia gharama zote za matibabu ya Dkt. Mvungi.
Tume inawaomba
wananchi wote waendelee kumuombea kwa Mungu Dr. Mvungi ili aweze kurejea katika hali
yake ya kawaida na hatimaye kuendelea majukumu yake.