Mheshimiwa Padre Galus Marandu, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya kufunga Mwaka
wa Imani kutoka Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania anabainisha kwamba, hadi sasa
maandalizi yamekamilika na wawakilishi kutoka majimbo mbali mbali wameanza safari
kuelekea Bagamoyo katika kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani n chini Tanzania
hapo tarehe 10 Novemba 2013.
Serikali imeridhia kutoa ulinzi na usalama kwa
waamini watakaoshiriki katika Maadhimisho ya Kufunga Mwaka wa Imani yanayoanza rasmi
tarehe 8 Novemba kwa njia ya semina za makundi ya Familia ya Mungu nchini Tanzania
na kilele chake ni hapo tarehe 10 Novemba 2013.
Baada ya kufunga kwa Mwaka
wa Imani, Familia ya Mungu nchini Tanzania itafanya tathmini ya kina kuhusu Mwaka
wa Imani na kwamba, Jumatatu tarehe 11 Novemba, 2013, washiriki wataanza kurejea tena
majimboni mwao, tayari kuwashirikisha na kumwilisha yale waliyojifunza kutoka Bagamoyo,
Mlango wa Imani.