Baba Mtakatifu Ijumaa jioni baada ya kuongoza Ibada ya Misa ya Maadhimisho ya Siku
ya Watakatifu wote, akiwa katika eneo la Makaburi ya Verano Roma, pia aliwakumbuka
marehemu wote na hasa walio fariki jangwani au baharini, hasa wahamiaji na wakimbizi
wakiwa katika harakati za kutafua njia mpya za kuboresha maisha yao.
Papa
alitoa sala ya utangulizi akisema, Tuombe. Ee Baba, uliye chanzo pekee cha utakatifu
wote , Mpendevu katika watakatifu wako wote, utuwezesha pia sisi kuufikia ukamilifu
wa upendo wako kupitia Ibada ya Ekaristi, inayo dumisha tumaini letu , wakati wa
hija yetu hapa duniani, tunapoielekea karamu ya mbinguni. Kwa njia ya Kristo Bwana
wetu. R. - Amina Kisha Papa aliendelea kusema, “ katika muda huu wa kutembelea
maeneo ya makaburi, waliko kupumzika ndugu zetu, wake kwa waume, pia unakuwa ni
wakati wa kutafakari hali yetu ya kiroho na kufanya upya imani yetu katika Kristo
ambaye alikufa , akazikwa na kufufuka tena kwa ajili ya wokovu wetu”. Papa alikumbusha,
hata miili iliyo kufa itatokea katika siku ya mwisho , na wale waliolala katika mapenzi
ya Bwana watahuishwa pamoja nae. Aliwasihi wote waliokuwa wamekusayika katika makaburi
hayo ya verano, kuinua maombi kwa Baba wa Mbinguni , kwa ajili ya Marehemu na kuomba
Baraka zake pia kwa ajili kila mmoja ili kwamba , baada ya kifo , wote waweze pia
kukutana mbele ya uso wa Bwana kwa furaha ya uzima wa milele.
Papa aliendelaa
kutoa Maombi na Baraka akisema, “Tubariki , Ee Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu
Kristo, katika huruma yako kubwa, tunafanywa upya kwa njia ya ufufuo wa Yesu
aliyetoka katika wafu, kwa tumaini hai , kwa ajii ya kutupatia urithi usio haribiki
wala kuoza ;”
“kiliza maombi yetu tunayokutolea wewe Bwana, kwa ajili ya wapendwa
wetu walio tutangulia kuondoka katika dunia hii : fungua mikono yako ya huruma, na
uwapokea wote katika utukufu kanisa Takatifu Yerusalemu. Na uwafariji wale walio
katika maumivu ya kujitenga na wapendwa wao, uwajazea tumaini kwamba Wafu wanaishi
ndani yako, na pia hata waliobaki kuzimuni, ipo siku watashiriki katika ushindi
wa Pasaka ya Mwana wako.
Papa alikamilisha maombi na baraza akisema , Ninyi
ambao katika hija ya Kanisa , mmekuwa ishara ya Mwanga wa Bikira Maria ,kwa njia ya
maombezi yake, mdumishe imani , ili kusiwe na kikwazo kinachotaka kubadili njia
iendayo kwake, Yeye aliye furaha isiyokuwa na mwisho.