2013-10-31 16:06:11

Wakristu wametakiwa kujua uthabiti wa upendo wao kwa Kristu.


Baba Mtakatifu Francisko , mapema Alhamis hii asubuhi , aliadhimisha Ibada ya Misa, katika madhabahu ya Mtakatifu Sebastian yaliyoko ndani ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro la Vatican, ambako mwili wa Mwenye Heri Papa Yohane Paulo Yohane II umehifadhiwa. Katika madhabahu hayo , kila siku ya Alhamis, kikundi cha waamini kutoka Poland hutolea sala zao katitika Madhabahu haya.Kwa Alhamis hii, mamia ya waamini wakiwemo Mapadre walihudhuria Ibada .
Homilia ya Papa ililenga katika barua ya Mtume Paolo kwa Warumi, ambamo Mtume Paulo anazungumzia upendo wa Kristu na aya za Injili , ambamo Yesu anaulilia mji wa Jerusalem alioupenda .
Papa Francisko, akitafakari kwa kina masono hayo anasema , mna sura mbili, zinazoonyesha njia mbalimbali za upendo huu unavyoweza kupokewa.
Kwa upande mmoja , alisema, tunapata uhakika wa upendo wa mtume Paulo kwa Yesu, kwa maneno yake anaposema, "hakuna mtu anayeweza kunitenga na upendo wa Kristo ". Mtume Paulo baada ya kuongoka, licha ya kuyaishi mateso ya mwili kwa njia mbalimbali, ugonjwa na usaliti, upendo wake kwa Kristo ulidumu kuwepo siku zote za maisha yake, hata saa mwisho ya kifo cha sulubu.
Na kwa upande mwingine, Francis Papa aliendelea , tunaiona huzuni ya Yesu, wakati alipowatazama watu wa Yerusalem walivyokosa uaminifu katika kuziishi sheria za Mungu. Moyo wa Yesu unaulilia mji huu, ulioshindwa kuuelewa upendo wa Mungu. upendo huo ambao haukupokelewa.

Papa Francisko alilinganisha sura hizi mbili, kwanza sura ya Paulo, ambaye anahisi yeye ni mwenye dhambi , lakini nguvu za imani yake zinatokana na kuupenda upendo wa Mungu, na sura ya Yerusalemu,ambao watu wake , wanashindwa kuukubali upendo wa Mungu na wengine wakiupokea kwa hali za mashaka mashaka, wakitawaliwa na ubinafsi wao.
Papa alizitafakari hali hizo na kutoa wito kwa kila Mkristu kujiuliza, je upendo wangu kwa Yesu ni thabiti kama wa Paulo au ni mashaka mashaka kama ilivyokuwa kwa watu Jerusalem?
Papa alieleza na kutoleo ombi kwa Mwenye Heri Yohane Paulo II, atusaidie kupata jibu linalo faa katika swali hili.








All the contents on this site are copyrighted ©.