2013-10-30 10:06:19

FAO inapania kuboresha ufugaji ili uwe wa tija na mafao kwa Jamii husika!


Bwana Josè Graziano da Silva, Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa Mataifa, FAO anasema, umefika wakati kwa Jumuiya ya Kimataifa kuunga mkono sera makini za wafugaji na wakulima vijijini, ili kupambana na ukame wa kutisha katika nchi za Sahel. Jumuiya ya Kimataifa haiwezi kuzuia ukame wala mafuriko, lakini inaweza kuwasaidia wakulima wafugaji kupambana na baa la njaa kutokana na mabadiliko ya tabianchi.

Wadau mbali mbali wako Kaskazini mwa Afrika ili kuangalia mikakati ya kilimo cha umwagiliaji kama njia ya kupambana na baa la njaa katika maeneo ya Sahel. Ukame wa kutisha umekuwa ni sababu ya kupanda kwa bei ya mazao ya chakula katika kipindi cha miaka ya hivi karibuni na hivyo kupelekea hali ya wasi wasi wa uhakika wa usalama wa chakula hasa miongoni mwa Jamii ya wafugaji, inayokadiriwa kuwa na watu millioni 16.

Hili ni kundi ambalo linahama hama kutafuta malisho na maji kwa ajili ya mifugo yake, lakini limekuwa ikipambana na ukame pamoja na mafuriko; mambo ambayo pia yameendelea kuchangia migogoro kati ya Jamii za wakulima na wafugaji Ukanda wa Sahel. FAO inataka kuwasaidia wafugaji ili waweze kuanza ufugaji bora utakaowapatia tija na kipato ili kuinua hali ya maisha ya familia zao.







All the contents on this site are copyrighted ©.