Askofu mkuu Job ang'atuka na Papa amemteua Askofu Osobo kuwa Askofu mkuu wa Jimbo
kuu la Ibadan
Baba Mtakatifu Francisko tarehe 29 Oktoba 2013, amekubali ombi la Askofu mkuu Felix
Alaba Adeosin Job wa Jimbo kuu la Ibadan, Nigeria kutoka madarakani kadiri ya sheria
za Kanisa Namba 401ยง 1.
Baba Mtakatifu ameteua Askofu Gabriel Leke Abegunrin
kuwa Askofu mkuu mteule wa Jimbo kuu la Ibadan. Kabla ya uteuzi huu, Askofu Abegunrin
alikuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki Osobo, Nigeria.