Balozi mpya wa Japan mjini Vatican awasilisha hati zake za utambulisho!
Baba Mtakatifu Francsiko, Jumatatu tarehe 28 Oktoba 2013 amepokea hati za utambulisho
kutoka wa Bwana Teruaki Nagasaki, Balozi mpya wa Japan mjini Vatican. Bwana Nagasaki
alizaliwa tarehe 4 Agosti 1952, ana mke na mtoto. Tangu mwaka 1977 alianza shughuli
zake katika masuala ya kidiplomasia na uhusiano wa kimataifa.
Taarifa zinaonesha
kwamba, amewahi kutekeleza wajibu huu kama mshauri wa kidiplomasia katika nchi mbali
mbali kama vile. Lima, Berna, Helsinki na Barcelona, Hispania. Kuanzia mwezo Agosti
2010 alikuwa ni Balozi wa Japan nchini Guatemala.