2013-10-26 08:59:40

Vatican na Serikali ya Hungaria watiliana sahihi itifaki ya ushirikiano!


Hivi karibuni, Vatican na Serikali ya Hungaria zilitiliana sahihi mkataba unaofanya mabadiliko katika itifaki iliyofikiwa hapo tarehe 20 Juni 1997, kuhusu ruzuku ya Serikali kwa huduma za kijamii zinazotolewa na Mashirika ya Kanisa Katoliki nchini Hungaria pamoja na baadhi ya masuala yanayohusiana na urithi wa kitamaduni.

Askofu mkuu Alberto Bottari, Balozi wa Vatican nchini Hungaria aliongoza ujumbe kutoka Vatican wakati ambapo ujumbe wa Serikali ya Hungaria uliongozwa na Dr. Bence Retvari, Katibu wa Bunge la Hungaria. Mabadiliko haya yanakwenda sanjari na Katiba ya nchi ya Mwaka 2011.

Katiba imefanya marekebisho kuhusu ruzuku inayotolewa na Serikali kwa Mashirika ya kidini, elimu ya dini shuleni pamoja na ukarabati wa sanaa za Kanisa ambazo ni sehemu ya urithi wa wananchi wa Hungaria. Itifaki hii itaanza kutekelezwa pale ambapo pende zote mbili zitaweza kuridhia vipengele vilivyomo kwenye mkataba huo!







All the contents on this site are copyrighted ©.