Baraza la Maaskofu Katoliki Angola, Sao Tome na Principe, linafunga Maadhimisho ya
Mwaka wa Imani, Jumapili tarehe 27 Oktoba 2013, katika Parokia ya Bikira Maria wa
Fatima. Sao Tome, kwa upande wake, itafunga Maadhimisho haya hapo tarehe 24 Novemba
2013.
Baraza la Maaskofu Katoliki Angola linaendelea na mkutano wake wa kawaida
wa Mwaka uliofunguliwa hapo tarehe 22 Oktoba na unatarajiwa kufungwa rasmi hapo tarehe
30 Oktoba 2013. Maaskofu kwa sasa wanapanga mikakati ya shughuli za kichungaji kwa
kipindi cha miaka mitatu ijayo.