Maandalizi ya Siku ya Wagonjwa Duniani kwa Mwaka 2016
Katika Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, Askofu mkuu Zygmunt Zimowski, viongozi waandamizi
kutoka Baraza la Kipapa la huduma kwa wafanyakazi wa sekta ya afya pamoja na kikundi
cha watu 80 wako Nchi Takatifu katika hija ya maisha ya kiroho. Tayari kikundi hiki
kimekwisha tembelea maeneo matakatifu na kuadhimisha Ibada ya Misa Takatifu pamoja
na kutembelea baadhi ya Hospitali katika maeneo hayo.
Askofu mkuu Zimowski
na ujumbe wake wanatarajia kuhitimisha hija hii ya maisha ya kiroho katika Maadhimisho
ya Mwaka wa Imani, Jumapili tarehe 27 Oktoba 2013. Hija hii ni sehemu ya maandalizi
ya Maadhimisho ya Siku ya Wagonjwa Duniani kwa Mwaka 2016 yatakayofanyika mjini Nazareth
kwa kuongozwa na kauli mbiu "Kujiaminisha kwa Yesu kama Bikira Maria, "Lolote atakalowaambia,
fanyeni".