Askofu Franz Peter wa Jimbo Katoliki Limburg asimamishwa uongozi kwa muda
Baba Mtakatifu Francisko baada ya kupewa taarifa rasmi kuhusu hali ya uchumi ya Jimbo
Katoliki la Limburg, Ujerumani na baada ya tafakari ya kina, ameamua kumsimamisha
katika uongozi wa Jimbo hilo, Askofu Franz Peter Tebartz-Van Elst. Baraza la Maaskofu
Katoliki Ujerumani kwa kushirikiana na viongozi wa Jimbo hilo wameunda kamati maalum
itakayochunguza tuhuma za ubadhirifu wa mali ya Kanisa kutokana na ukarabati wa makao
makuu ya Jimbo hilo.
Askofu Franz kwa sasa atakuwa nje ya Jimbo ili kutoa
nafasi kwa kamati hii kufanya uchunguzi wa kina na nafasi yake kwa sasa itakaimiwa
na Monsinyo Stadtdekan Wolfgan Rosch, makamu Askofu Jimbo Katoliki la Limburg katika
kipindi chote cha kutokuwepo kwa Askofu wa Jimbo hilo.