Kardinali Gianfranco Ravasi Rais wa Baraza la Kipapa la Utamaduni amewapongeza waamini
na watu wenye mapenzi mema walioshiriki katika mbio za mita 100 ya imani zilizofanyika
kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, Jumapili tarehe 20 Oktoba
2013 kama sehemu ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani.
Hii inaonesha kwamba, kuna
uhusiano wa karibu kati ya imani na michezo na kwamba, michezo inamwezesha mwamini
kutolea ushuhuda wa imani yake kwa Mwenyezi Mungu, ambaye ni mwingi wa huruma na mapendo.
Imani ni hazina muhimu inayomwezesha mwamini kufanya majadiliano ya kina na michezo
ambayo kila mtu anashiriki kwa kadiri ya kiwango na nafasi yake.
Ni changamoto
kwa waamini na watu wenye mapenzi mema kuhakikisha kwamba, michezo inakuwa ni sehemu
ya furaha, amani, upendo na mshikamano wa kidugu unaowachangamotisha wanamichezo kuondokana
na ubinafsi wao na matendo ambayo ni kinyume cha dhana ya michezo.