2013-10-19 11:26:05

ICC yatoa msamaha kwa Rais Uhuru Kenyatta


Majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita, ICC, mwishoni mwa juma, imetoa msamaha kwa Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya anayekabiliwa na mashitaka ya mauaji ya watu zaidi ya 1200 yaliyotokea kunako mwaka 2007 mara baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya kwamba, kwa sasa hatalazimika tena kuwepo wakati wote Mahakamani hapo wakati wa kusikiliza kesi yake inayomhusisha pia Makamu wa Rais wa Kenya Bwana William Ruto. Kesi hii inatarajiwa kuendelea kusikilizwa tena, mwezi Novemba, 2013.

Uamuzi huu ni matokeo ya shinikizo kutoka kwa viongozi wa Umoja wa Afrika ambao wamekuwa wakitishia kujitoa katika Mahakama hii kutokana na ICC kuendelea kuwakandamiza viongozi kutoka Afrika, hali ambayo ingegumisha mchakato wa mapambano dhidi vitendo vya kigaidi Barani Afrika. Hivi karibuni nchi za Magharibi zilimshauri Rais Uhuru Kenyatta kuonesha ushirikiano wa dhati na Mahakama ya Kimataifa, kwani Kenya ina mchango mkubwa katika mchakato dhidi ya vitendo vya kigaidi Barani Afrika.







All the contents on this site are copyrighted ©.