2013-10-18 13:34:56

Rais Paul Biya akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko, Ijumaa tarehe 18 Oktoba 2013 amekutana na kuzungumza na Rais Paul Biya, Rais wa Cameroon ambaye pia alikutana na Askofu mkuu Dominique Mamberti, katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Viongozi hawa wawili katika mazungumzo yao wamepongeza uhusiano mzuri uliojengeka kati ya Vatican na Cameroon na kwamba, kwa pamoja wameonesha matumaini katika mchakato unaotaka kuhitimisha mkataba kati ya Vatican na Cameroon kuhusu nafasi ya Kanisa Katoliki kisheria nchini Cameroon. Makubaliano haya yanatarajiwa kutiwa sahihi katika kipindi cha siku chache zijazo!

Viongozi hao wamelipongeza Kanisa Katoliki nchini Cameroon kutokana na mchango wake kwa wananchi katika medani mbali mbali za maisha, hususan katika sekta ya elimu, afya; haki, amani na upatanisho.

Baba Mtakatifu Francisko na Rais Paul Biya wamegusia pia changamoto ambazo Bara la Afrika linaendelea kukabiliana nazo sanjari na mchango wa Cameroon katika kuimarisha mchakato wa amani na uptanisho Barani Afrika.








All the contents on this site are copyrighted ©.