Baba Mtakatifu Francisko katika Maandalizi ya Siku kuu ya Pasaka kwa Mwaka 2014, ataungana
na wasaidizi wake wa karibu kwa ajili ya Mafungo ya Kipindi cha Kwaresima, ambayo
kwa Mwaka 2014 yatafanyika kuanzia tarehe 9 Machi hadi tarehe 14 Machi 2014 mjini
Albano, nje kidogo ya mji wa Roma. Mafungo haya yataongozwa na Monsinyo Angelo De
Donatis kutoka Jimbo kuu la Roma.
Habari hizi zimethibitishwa na Padre Federico
Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican na kwamba, lengo na kufanya mafungo haya ya kiroho
nje ya mji wa Vatican ni kuwawezesha wahusika wakuu kupata nafasi ya ukimya na utulivu
ili waweze kupata nafasi ya kusali, kutafakari na kufunga; mambo msingi katika hija
ya maisha ya kiroho kwa waamini.