Katekesi ya Papa- Tunasadiki katika Kanisa moja la Kitume kwa sababu.....
Katekesi ya Baba Mtakatifu Francisko kwa mahujaji na wageni, inaendelea kuitafakari
sala ya Kanisa, ya Nasadiki, Jumatano hii akitazama kifungu Nasadiki katika Kanisa
moja Takatifu na la Kitume. Na alianza kwa kuwahoji mahuajii na wageni wanaofika Roma
kwa ajili ya hija , iwapo wamewahi kujiuliza ina maana gani kusema , Kanisa la Mitume
na umuhimu wa Mitume Petro an Paulo, ambao waliyatoa maisha yao hapa Roma , kwa
ajili ya kuifikisha Injili na kuishuhudia Injili . Lakini pia akasema, kuna zaidi
katika hilo....
Papa alieleza na kusisitiza kwamba Kanisa la kitume, kwa sababu,
lina uhusiano kina, katika urithi wake na Mitume kwa kwanza, lile kundi dogo la wanaume
kumi na wawili walioitwa na Yesu kwa majina na kuishi nae na hatimae kuwatuma nje
kuhubiri mafundisho yake ( Mk 3:13-19 ).
Papa alieleza na kufafanua maana
ya neno “Apostolo” Mtume , kwamba ni neno la Kigiriki lenye maana ya "aliyetumwa
", ni mtu anayepeleka ujumbe wa kufanya jambo fulani. Ni neno lenye nguvu , na
Mitume waliitwa na kuchaguliwa na Yesu kuendeleza kazi yake , ya kusali na kupeleka
habari njema ya upendo wa kuokoa kwa watu wote. Hivyo sala na kutangaza Injili ,
inakuwa ni kazi ya kwanza muhimu ya mtume.. Papa ametaja hili ni muhimu kwa sababu,
mara nyingi , wengi tunafikiri, kuwa mtume ni kwenda kuihbiri injili peke yake. Sivyo,
ni kufanya kazi nyingi ... Papa alifafanua, na kurejea siku za mwanzo wa Kanisa,
akisema, pia kulikuwa na matatizo na vikwazo kwa mitume kulingana na wakati wao.
Na hivyo walitayarisha watu wengine kama mashemasi, katika kukabilaina na kupungukiwa
na wakati wa kuomba na kutangaza Neno la Mungu. Na kama tunavyo fikiri juu waandamizi
wa Mitume - Maaskofu, na pia Papa,ambao nao pia wana tatizohili la kupungukiwa na
muda wa kusali na kuitangaza Injili kama warithi wa mitume. kwa muono huo, Papa Francisko
amesisitiza, kila muumini wa kanisa ni mtume, kwa sababu yumo ndani ya Kanisa la
kitume. Na hivyo waamini wote wanatakiwa kuwa mitume katika kazi yake ya kuihubiri
Injili ya wokovu wa ulimwengu. Papa alieleza na kutaja mambo matatu katiak mafundisho
yake kwamba, Kanisa ni la kitume kwa sababu, limejengwa juu ya maombi na mahubiri
ya Mitume, kwa mamlaka yalitolewa kwa mitume na Kristo mwenyewe,kama alivyoandika
Mtakatifu Paulo kwa Wakristo wa Efeso (2, 19-20) . Pili Kanisa ni la kitume
kwa sababu hudumisha ukamilifu wa mafundisho ya Kristu na njia za wokovu, kwa msaada
wa Roho Mtakatifu , kama inavyo eleza Kateksimu ya Kanisa. Kanisa karne hadi karne
limetunza hazina hii ya thamani, ambayo ni maandiko matakatifu , mafundisho , sakramenti,
huduma ya wachungaji, ili twaamini waweze kuwa waaminifu kwa Kristo na kuyashiriki
maisha yake. Na tatu Kanisa ni la kitume kwa sababu, ujumbe wake uliodmanishwa
kwa mitume ni ujumbe wa injili kwa dunia nzima, unaoendelea katika njia ya historia
ya ujumbe huo, ambao Yesu aliukabidhi Mitume. Yesu mwenyewe alisema, nendeni mkawafanye
mataifa yote kuwa wanafunzi wangu, mkiwabatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la
Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi . Na tazama, mimi
nipo pamoja nanyi siku zote , mpaka mwisho wa ulimwengu "( Mt 28:19-20). Na hivyo
Kanisa mizizi yake imo katika mafundisho ya Mitume, mashahidi wa kweli wa Kristo.
Hivyo , leo tunapaswa kufurahia na kulipenda kanisa kama ni mahali pa kukutana na
Bwana Mfufuka , aliyewatuma mitume wake , kuwaalika wote waliokutana nao kuufahamu
ukweli wa Injili , furaha ya imani na ahadi ya maisha ya Milele, iliyotangazwa na
Mitume.