Hotuba ya Kardinali Tarcisio Bertone kwa Papa wakati akiaga rasmi cheo cha Katibu
wa Jimbo la Papa
Kardinali Tarcisio Bertone, katika kuhitimisha utume wa kuwa Katibu wa Jimbo la Papa
, Oktoba 15, 2013, aliagana na Papa Francisko, kwa maneno yaliyotoka ndani ya roho
ya Wasalesiano , na pia kwa Mtakatifu Ignatius wa Loyola, na pia kwa moyo wa Don
Bosco. Kardinali Bertone aliagana na Papa wakiwa katika Chumba cha Mkitaba ya Papa,
mjini Vatican , ambamo Kardinali alitoa shukurani zake dhati wa Papa Francisko, akisema,
asante sana. Na aliainisha kuhitimisha kwa majukumu yake kama Katibu wa Jimbo
la Papa sanjari na Hija Fatima, katika maadhimisho ya tukio la Mwisho la Bikira
Maria kuwatokea watoto wa Fatima , na pia kwa ajili ya kutimia miaka 60 tangu kujengwa
kwa Basilika la Rozari Takatifu Fatima, kama alivyosema muumini mmoja, kwenda kwake
katika madhabahu hayo, kuhitimisha kazi yake ya kuwa Katibu, ilikuwa sawa na kukabidhi
ufunguo wa dhahabu.
Kardinali Bertone, katika maelezo yake amekiri, ni
ngumu kwake kutoa muhtasari wa kina juu ya miaka saba ya utumishi wake kama Katibu
kwa Papa Benedict XVI na, kwa kipindi kifupi cha Papa Francisko. Lakini ametaja mambomuhimu
aliyoyaweka moyoni mwake kama kumbukumbu, ni umuhimu wa kufanya kazi kwa ukaribu
na kila mtu, katika ufanikishaji wa kazi pamoja , licha ya kuwa na majukumu tofauti
na majitoleo binafsi ambayo wakati mwingine ni sadaka. Kardinali ametoa shukurani
zake kwa wote.
Kardinali alieleza pia kilichomvutia kwa Papa Benedict XVI,
ni mtazamo na uelewa wake wa juu Kanisa kama ni ushirika katika kina kirefu, na
pia uwezo wake katika kuzungumza na ulimwengu na kugusa mioyo na akili ya watu wengi,
kupitia mafundisho yake yenye uwazi na kina cha fikira. Na kwamba Papa Benedict
XVI alikuwa ni mtengenezaji wa majiundo ya dhamiri na Makleri. Utawala wake kama
Papa , uiliweka nguvu zaidi katika utume wa kichungaji, kwa kuwa na matukio kadhaa
muhimu kama kuitisha Mwaka Mtakatifu Paulo, Mwaka kwa ajili ya Mapadre, na Mwaka
wa imani. Karidinali Bertone pia amedokeza vipindi vigumu vilivyo umiza moyo wa
Papa Benedikto XV1, kwa ndani kwamba ni uchungu kwa maovu yanayochafua sura nzuri
ya Kanisa. Na kwa ajili ya kutunza utakatifu wa Kanisa, aliweka sheria mpya, katika
kukabiliana na hali ya aibu ya viongozi wabovu wa kanisa, wenye kuchafua uso wa kanisa
kama kasha ya madhulumu ya kijinsia kwa watoto. Pia bila ya kusahau uzinduzi wa
sheria mpya ya kiuchumi na kiutawala kwa jimbo la Papa . Na kwamba , Bwana alimwongoza
katika uvuvio wa kiroho, baada ya kutafakari na maombi ya makali ya kina, alichukua
uamuzi wa kujiondoa katika huduma utume wa Petro, kama alivyoongozwa na Roho wa Yesu.
Kardinali Bertone pia alitaja kwa muhtasari juu ya Papa Francesko, akisema, juhudi
anazozifanya si kwamba anafanya mapinduzi, lakini anaendeleza mawazo ya Papa Benedilto
XVI, kwa utajiri wa utofauti wa lugha na uzoefu wa maisha, kulingana na asili yetu
na njia yetu, kama yeye mwenyewe Papa Francisko anavyosema , tuko pamoja katika utajiri
wa utofauti wetu. Na maelewano ni jambo la msingi na njema. Kusikiliza , huruma,
rehema, na imani maajabu ya ukweli kwamba, ambao Papa Francisko yeye mwenyewe binafsi
anauzoefu nao, kama anavyoendelea kueleza katika mazungumzo yake.
Na amemshukuru
Papa Francisko kwa wema wake! Na ameomba kwa Maria, awe msaada daima kwake Yeye
Papa Francisko na Katibu mpya wa Jimbo, Mheshimiwa Askofu Mkuu Monsignor Pietro Parolin
, ili kanisa zima la Ulimwengu lipate kufungua mafundo yote yanayozuia bado Kanisa
la Kristo, kuwa katika moyo wa upeo wa macho ya dunia zima, ambalo ni ombi la kina
kwetu sote. Asante, Baba Mtakatifu!