Baraza la Mawaziri Malawi lavunjwa kwa rushwa na ufisadi!
Rais Joyce Banda wa Malawi, mwishoni mwa juma amevunja Baraza la Mawaziri kwa tuhuma
za kujihusisha na ubadhirifu wa mali ya umma pamoja na ufisadi. Uamuzi wa Rais Banda
unatokana na manung’uniko ya wananchi kwa Mawaziri 25 kwamba walikuwa wanajihusisha
na vitendo vya rushwa na ufisadi, hali iliyopelekea wafadhili wakuu wa Malawi kutishia
kusitisha misaada yake nchini Malawi, ikiwa kama Rais Joyce Banda angeshindwa kuchukua
hatua za kinidhamu dhidi ya Mawaziri wake.
Wakati huo huo, Rais Banda ameunda
tume maalum ili kuchunguza fedha ya umma na kwamba, masuala ya mambo ya nchi za nje
na ushirikiano wa kimataifa kwa sasa yatasimamiwa na Ofisi ya Rais hadi pale mawaziri
wapya watakapokuwa wameteuliwa tena.