2013-10-14 15:18:00

Jinsi nina hamu ya Kanisa kuwa maskani kwa ajili ya maskini!”


Kwa maneno haya aliyoyatamka mara tu baada ya kuchaguliwa kwake kama Baba Mtakatifu, Jorge Bergoglio aliigusia mada ambayo imeendelea kuwa ndicho kipaumbele cha kwanza na kiini cha uongozi wake kama Papa. Si kitu cha kushangaza kwamba watu wengi wamesema kwamba maneno kama haya yanaonyesha kwamba Baba Mtakatifu Francisko anawataka wakatoliki kuwa makini na kutolea muda wao katika mchakato wa kupambana na baa la umaskini. Kwa upande mmoja, haya ni kweli. Hata hivyo ni tafsiri iliyopungukiwa na maana halisi na ya ndani zaidi ambayo Francis mwenyewe anaiambatanisha na umaskini.

Mtu yeyote hapaswi kushangaa kwamba Francis anaongea sana juu ya hali ya umaskini, kwani yeye mwenyewe ni mwenyeji wa Amerika ya Kusini: sehemu ya ulimwengu ambapo mamilioni ya watu (isipokuwa Chile) wanaishi kwenye umaskini mkuu. Utakuwa umekosa utu usipoguswa na tofauti za kutisha kati ya Recoleta ambao ni mji mzuri na wa kupendeza wa Buenos Aires, unao ufanya mji huo kujulikana kama Paris ya Kusini, na hali duni ya maisha ya vitongoji kama vile Rodrigo Bueno.

Wakristo hawana budi kuguswa na tofauti kama hizi. Lakini ili tuyaelewa maneno ya Francis juu ya umaskini lazima tuelewe kwamba Baba Mtakatifu ni Mkatoliki haswa. Yeye sio mwanafalsafa au mchumi mtendaji (practical materialist). Kwa hivyo, ung’amuzi wa Papa Francisko juu ya maskini na umaskini unapita ule uelewa wa kawaida wa kijamii kuhusiana na maswala haya.

Katika cha kusisimua cha maswali na majibu kwenye vigilia ya Pentekoste ya mwaka huu, pamoja na washiriki wa vyama vipya katika Kanisa (new movements) ambavyo vimechangia sana kuleta uhai ndani ya Kanisa tangu Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, Baba Mtakatifu aliyasema haya kuhusu Ukristo na Umaskini.

Kwetu Wakristo umaskini sio swala la kijamii, kifalsafa au kitamaduni. La hasha, bali ni swala la kiteologia. Ningesema pengine swala la kwanza, kwani Mungu Mwana alijishusha, akajifanya maskini ili kuweza kuambatana nasi kwenye njia yetu. Na huu ndio umaskini wetu: umaskini wa mwili wa Kristo, umaskini ambao mwana wa Mungu alituletea kwa kujifanya mtu kwake. Kanisa maskini kwa ajili ya maskini linaanza kwa kuuelekea mwili wa Kristo. Tukiuelekea mwili wa Kristo, tutaanza kuelewa kitu, kumbe tutaelewa maana hasa ya umaskini huu, umaskini wa Bwana.

Kwa neno moja, hili linagusia unyenyekevu. Kama Myesuiti mwingine, Philip Caraman, alivyoandika wakati mmoja, unyenyekevu ni fadhila “ambayo kwayo tunajipima kisawasawa mbele ya Mungu, tukitilia maanani yote yale ambayo Mungu ametupa, ametufanyia, na anayotarajia kutoka kwetu.”

Uelewa mwingine unatokana na kukumbuka kwamba neno la Kigiriki lililotumiwa kwenye Injili ya Mathayo(5:3) kuelezea “umaskini wa kiroho” (πτωχός) lina maana ya kushushwa hadi kuwa mwombaji. Kwa sababu hiyo, maskini wa kiroho ni wale kati yetu – maskini, tajiri, wenye kipato cha kati – wenye kuzifahamu dhambi zetu na kumwomba Kristo atuokoe.

Hiki ndicho kiini cha nini hasa maana ya Kanisa Maskini. Kanisa nyenyekevu sio Kanisa lenye uoga, lenye waumini wenye kunyong’onyea kwenye mambo ya imani; bali ni Kanisa ambalo linawajumuisha watu ambao, kwa uhuru kabisa, wanajitoa kidete kwa Kristo aliye peke yake mwenye uwezo wa kutuokoa.

Hayo pia yanajiri kwenye tafakari juu ya maisha ya Mtakatifu Francisko wa Assisi. Hapa ni vizuri kuonesha pengo lililopo kati ya riwaya zisimuliwazo juu ya Francisko, na ukweli hasa juu ya mtu huyu.

Kwa mfano, katika wake wa hivi karibuni juu ya Francisko, Mdominikani Augustine Thompson, anaonyesha kwamba mazungumzo yaliyosifika sana kati ya Francisko na Sultan al-Kamil wa Misri hayakuchangiwa na hisia zozote au harakati dhidi ya vita. Kwake Francisko, lengo la tendo hili lilikuwa kumbadilisha Sultan huyo kuwa Mkristo!

Pia Thompson anaonyesha ukosefu wa subira wa Francisko juu ya ulegevu kwenye maswala ya Kiliturjia, ukosefu wake wa kujihusisha na aina yoyote ile ya programu za kisheria au mageuzi ya kijamii, uwezo wake wa kubainisha kati ya umaskini hohe hahe na ule wa kawaida, na pia hakushikilia itikadi na fikira zilizojiri kwa wakati wake kuhusiana na Mungu na Mazingira au Pantheism kwa lugha ya Kimombo; na kwamba kitu asichokuwa akitazamia kabisa Francisko ni kwa shirika lake kugeuka kuwa kikundi cha wafanyakazi wa kijamii au social workers. Mtakatifu Francisko, anaendelea kusema Thompson, alikuwa mkakamavu wa imani, na kwamba Francisko alikuwa mtii kwa Mungu na Kanisa, akimaanisha uongozi wake mathubuti.” Katika wosia wake wa mwisho, Fransisko hata alisisitiza kwamba waasi au wakiukaji wa sheria ambao wangejitokeza kwenye shirika lake watolewe kwa serikali ili iwashughulikie kulingana na sheria za nchi.

Kutokana na yote haya, inakuwa vigumu kumwona Francisko kama mpinzani, au mtetezi na mwanaharakati wa namna yoyote ile. Hata Wakatoliki wengine hushangaa wanapogundua kwamba uelewa wa Francisko juu ya umaskini haukuwa unapinga tofauti za kijamii juu ya kipato au kuwaonea wivu matajiri. Thompson anaonyesha kuwa Mtakatifu huyu aliandika kidogo sana juu ya umaskini, na wakati alipoandika, haikuwa na uhusiano na “kujibandua kabisa na mali, maisha ya kawaida, au kuishi tu kwa siku hiyo.” Bali ilikuwa hasa kuhusiana na ukweli kuhusu Nafsi ya Pili ya Utatu Mtakatifu aliyejishusha na kuchukua hali ya kibinadamu katika umwilisho na kujitoa sadaka kwa ajili ya binadamu wote kwa kufa Msalabani.

Kwa hiyo, kulingana na Thompson, mtazamo wa Mtakatifu Francisko kuhusu umaskini ulikuwa hasa ni “kujikana mwenyewe, kutoa huduma kwa ajili ya Mungu na kuyatii Maandiko Matakatifu yanayohubiriwa na Kanisa la Kristo. Kwa maana hiyo, mawazo ya Francisko kuhusiana na umaskini, kama alivyoandika Thompston , siyo ya “kisiasa.” Ila ni kuhusu kuufikia utajiri wa kiroho unaotokana na kumkumbatia hasa Kristo.

Je, hili linatuambia nini kuhusiana na jinsi wakatoliki wanapaswa kuwaza juu ya umaskini?
Kwanza kabisa, ukereketwa wa kisiasa usiwe ndicho kitu cha kwanza kufikiria tunapoongea juu ya kukomesha umaskini. Sio bure kwamba Baba Mtakatifu Francisko kwenye mahubiri yake ya vigilia ya siku ya Pentecost alisisitiza kwamba “Kanisa sio mfumo wa kisiasa, au chama fulani, na kwamba kama Kanisa... sisi si Shirika lisilo la Kiserikali (NGO), na kwamba, Kanisa linapokuwa NGO, linapoteza chumvi na ladha yake, na hivyo linabaki kama chama tu, bila uhai.”

Ni kweli kwamba wa Baba Mtakatifu Francisko kwa serikali kuzingatia majukumu yao hasa kuhusiana na maswala ya uchumi wa kimataifa, unatokana na uhakika wake kwamba kuna jukumu la kisiasa katika kukabiliana na umaskini. Ila maandishi yake kabla ya kuchaguliwa kuwa Papa yanabainisha kwamba Francisko analiona hili kwani hapo 2011 (wakati uchumi wa Argentina ulipoanguka), Bergolio aliandika kwenye jarida la , kwamba “kuna waagentina wanaokumbwa na umaskini na kusukumwa pembezoni mwa jamii, ambao ni lazima tuwachukulie kama wadau na wahusika katika kuchonga hatima ya maisha yao wenyewe, na sio tu kama wafaidi wa misaada inayotolewa na serikali na mashirika ya kijamii”.

Lakini zaidi ya yote Francisko anawataka wakatoliki kuonyesha mwanga wa kikristo katika kukabiliana na swala la umaskini. Katika hotuba yake ya vigilia ya Pentekoste, alisisitiza kwamba lengo letu la kwanza lisiwe nguvu tendaji na kufanikiwa. “Ni kitu kimoja kumhubiri Yesu,” Francisko aliwaambia wasikilizaji wake, “na kitu kingine kufanikiwa.”

Haimaanishi kwamba wakristo hawana wajibu wa kufikiri na hata kujadiliana jinsi ya kuukomesha au kuupunguza umaskini. Ndivyo inavyodai haki. Francisko anataka kutuonyesha kwamba ikiwa tutashughulikia tu “mafanikio kwa mtazamo wa kidunia”, kuna hatari ya kuusahau upendo wa Kikristo.

Katika kuendeleza mjadala wake, Papa Francisko aliwauliza maswali mawili wale waliokuwa wakimsikiliza: “Niambieni, unapomsaidia mtu aneyeomba njiani, unamwangalia machoni baba au mama huyo?. . . Na unapomsaidia, unamshika mkono unayemsaidia au unamrushia tu vishilingi?”
Mambo matatu—kama asemavyo Francisko!—yanajitokeza hapa. Moja ikiwa ni: mara ngapi sote tumeanguka mtihani huu?

Pili ni Mwenyeheri Theresa of Calcutta. Hakuwa na mawazo ya kufanikiwa alipoamua kuwahudumia walio hoi zaidi miongoni mwa watu wa dunia. Katika maisha yake, alikaripiwa kwa kutokujihusisha zaidi kisiasa kuhusu baa la umaskini. Ila kazi yake haikuwa ya kisiasa. Ilikuwa juu ya kitu ambacho ni kikuu kuliko siasa: kuuleta upendo wa Kristo kwa wale ambao Kristo mwenyewe alituambia tutauona uso wake ndani mwao.

Na tatu ni kile ambacho Papa mstaafu Benedicto XVI alisisitizia sana kwenye waraka wake wa kwanza wa kipapa, , Mungu ni Upendo. Ijapokuwa waraka huu ulisisitiza sana maswala ya haki, Benedict wa kumi na sita alikazia kwamba kuna kitu ambacho kila mtu anayekumbwa na mateso anakihitaji zaidi: “upendo wa kipekee na kuthaminiwa.”

Kwao Baba Mtakatifu Francisko, mtangulizi wake (Benedikto wa kumi na sita), na Mwenye heri Mama Theresa (Wa Calkutta), jibu letu kuhusiana na umaskini lazima liwe, juu ya yote, kuonyesha haswa huruma, ambayo ndiyo kiini cha Injili. Pamoja na mambo mengine, hii inasaidia kusahihisha ule mwelekeo wa kibinadamu kwamba haki tu inatosha. Mungu angekuwa ni Haki tu, bila Upendo asingeweza kushuka na kuingia kwenye historia ya wanadamu kwa umbo la Yesu Kristo ili kutuokoa kutokana na sisi wenyewe. Tulikuwa hatumdai Mungu chochote. Kwa maana hiyo, basi, uelewa wa Kikatoliki kuhusu umaskini unatukumbusha kwamba ni Huruma ya Kimungu, na sio haki, ambayo inatuokoa.

Kwa maneno haya aliyoyatamka mara tu baada ya kuchaguliwa kwake kama Baba Mtakatifu, Jorge Bergoglio aliigusia mada ambayo imeendelea kuwa ndicho kipaumbele cha kwanza na kiini cha uongozi wake kama Papa. Si kitu cha kushangaza kwamba watu wengi wamesema kwamba maneno kama haya yanaonyesha kwamba Baba Mtakatifu Francisko anawataka wakatoliki kuwa makini na kutolea muda wao katika mchakato wa kupambana na baa la umaskini. Kwa upande mmoja, haya ni kweli. Hata hivyo ni tafsiri iliyopungukiwa na maana halisi na ya ndani zaidi ambayo Francis mwenyewe anaiambatanisha na umaskini.

Mtu yeyote hapaswi kushangaa kwamba Francis anaongea sana juu ya hali ya umaskini, kwani yeye mwenyewe ni mwenyeji wa Amerika ya Kusini: sehemu ya ulimwengu ambapo mamilioni ya watu (isipokuwa Chile) wanaishi kwenye umaskini mkuu. Utakuwa umekosa utu usipoguswa na tofauti za kutisha kati ya Recoleta ambao ni mji mzuri na wa kupendeza wa Buenos Aires, unao ufanya mji huo kujulikana kama Paris ya Kusini, na hali duni ya maisha ya vitongoji kama vile Rodrigo Bueno.
Wakristo hawana budi kuguswa na tofauti kama hizi. Lakini ili tuyaelewa maneno ya Francis juu ya umaskini lazima tuelewe kwamba Baba Mtakatifu ni Mkatoliki haswa. Yeye sio mwanafalsafa au mchumi mtendaji (practical materialist). Kwa hivyo, ung’amuzi wa Papa Francisko juu ya maskini na umaskini unapita ule uelewa wa kawaida wa kijamii kuhusiana na maswala haya.

Katika cha kusisimua cha maswali na majibu kwenye vigilia ya Pentekoste ya mwaka huu, pamoja na washiriki wa vyama vipya katika Kanisa (new movements) ambavyo vimechangia sana kuleta uhai ndani ya Kanisa tangu Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, Baba Mtakatifu aliyasema haya kuhusu Ukristo na Umaskini.

Kwetu Wakristo umaskini sio swala la kijamii, kifalsafa au kitamaduni. La hasha, bali ni swala la kiteologia. Ningesema pengine swala la kwanza, kwani Mungu Mwana alijishusha, akajifanya maskini ili kuweza kuambatana nasi kwenye njia yetu. Na huu ndio umaskini wetu: umaskini wa mwili wa Kristo, umaskini ambao mwana wa Mungu alituletea kwa kujifanya mtu kwake. Kanisa maskini kwa ajili ya maskini linaanza kwa kuuelekea mwili wa Kristo. Tukiuelekea mwili wa Kristo, tutaanza kuelewa kitu, kumbe tutaelewa maana hasa ya umaskini huu, umaskini wa Bwana.

Kwa neno moja, hili linagusia unyenyekevu. Kama Myesuiti mwingine, Philip Caraman, alivyoandika wakati mmoja, unyenyekevu ni fadhila “ambayo kwayo tunajipima kisawasawa mbele ya Mungu, tukitilia maanani yote yale ambayo Mungu ametupa, ametufanyia, na anayotarajia kutoka kwetu.”

Uelewa mwingine unatokana na kukumbuka kwamba neno la Kigiriki lililotumiwa kwenye Injili ya Mathayo(5:3) kuelezea “umaskini wa kiroho” (πτωχός) lina maana ya kushushwa hadi kuwa mwombaji. Kwa sababu hiyo, maskini wa kiroho ni wale kati yetu – maskini, tajiri, wenye kipato cha kati – wenye kuzifahamu dhambi zetu na kumwomba Kristo atuokoe.

Hiki ndicho kiini cha nini hasa maana ya Kanisa Maskini. Kanisa nyenyekevu sio Kanisa lenye uoga, lenye waumini wenye kunyong’onyea kwenye mambo ya imani; bali ni Kanisa ambalo linawajumuisha watu ambao, kwa uhuru kabisa, wanajitoa kidete kwa Kristo aliye peke yake mwenye uwezo wa kutuokoa.

Hayo pia yanajiri kwenye tafakari juu ya maisha ya Mtakatifu Francisko wa Assisi. Hapa ni vizuri kuonesha pengo lililopo kati ya riwaya zisimuliwazo juu ya Francisko, na ukweli hasa juu ya mtu huyu.

Kwa mfano, katika wake wa hivi karibuni juu ya Francisko, Mdominikani Augustine Thompson, anaonyesha kwamba mazungumzo yaliyosifika sana kati ya Francisko na Sultan al-Kamil wa Misri hayakuchangiwa na hisia zozote au harakati dhidi ya vita. Kwake Francisko, lengo la tendo hili lilikuwa kumbadilisha Sultan huyo kuwa Mkristo!

Pia Thompson anaonyesha ukosefu wa subira wa Francisko juu ya ulegevu kwenye maswala ya Kiliturjia, ukosefu wake wa kujihusisha na aina yoyote ile ya programu za kisheria au mageuzi ya kijamii, uwezo wake wa kubainisha kati ya umaskini hohe hahe na ule wa kawaida, na pia hakushikilia itikadi na fikira zilizojiri kwa wakati wake kuhusiana na Mungu na Mazingira au Pantheism kwa lugha ya Kimombo; na kwamba kitu asichokuwa akitazamia kabisa Francisko ni kwa shirika lake kugeuka kuwa kikundi cha wafanyakazi wa kijamii au social workers. Mtakatifu Francisko, anaendelea kusema Thompson, alikuwa mkakamavu wa imani, na kwamba Francisko alikuwa mtii kwa Mungu na Kanisa, akimaanisha uongozi wake mathubuti.” Katika wosia wake wa mwisho, Fransisko hata alisisitiza kwamba waasi au wakiukaji wa sheria ambao wangejitokeza kwenye shirika lake watolewe kwa serikali ili iwashughulikie kulingana na sheria za nchi.

Kutokana na yote haya, inakuwa vigumu kumwona Francisko kama mpinzani, au mtetezi na mwanaharakati wa namna yoyote ile. Hata Wakatoliki wengine hushangaa wanapogundua kwamba uelewa wa Francisko juu ya umaskini haukuwa unapinga tofauti za kijamii juu ya kipato au kuwaonea wivu matajiri. Thompson anaonyesha kuwa Mtakatifu huyu aliandika kidogo sana juu ya umaskini, na wakati alipoandika, haikuwa na uhusiano na “kujibandua kabisa na mali, maisha ya kawaida, au kuishi tu kwa siku hiyo.” Bali ilikuwa hasa kuhusiana na ukweli kuhusu Nafsi ya Pili ya Utatu Mtakatifu aliyejishusha na kuchukua hali ya kibinadamu katika umwilisho na kujitoa sadaka kwa ajili ya binadamu wote kwa kufa Msalabani.

Kwa hiyo, kulingana na Thompson, mtazamo wa Mtakatifu Francisko kuhusu umaskini ulikuwa hasa ni “kujikana mwenyewe, kutoa huduma kwa ajili ya Mungu na kuyatii Maandiko Matakatifu yanayohubiriwa na Kanisa la Kristo. Kwa maana hiyo, mawazo ya Francisko kuhusiana na umaskini, kama alivyoandika Thompston , siyo ya “kisiasa.” Ila ni kuhusu kuufikia utajiri wa kiroho unaotokana na kumkumbatia hasa Kristo.

Je, hili linatuambia nini kuhusiana na jinsi wakatoliki wanapaswa kuwaza juu ya umaskini?
Kwanza kabisa, ukereketwa wa kisiasa usiwe ndicho kitu cha kwanza kufikiria tunapoongea juu ya kukomesha umaskini. Sio bure kwamba Baba Mtakatifu Francisko kwenye mahubiri yake ya vigilia ya siku ya Pentecost alisisitiza kwamba “Kanisa sio mfumo wa kisiasa, au chama fulani, na kwamba kama Kanisa... sisi si Shirika lisilo la Kiserikali (NGO), na kwamba, Kanisa linapokuwa NGO, linapoteza chumvi na ladha yake, na hivyo linabaki kama chama tu, bila uhai.”

Ni kweli kwamba wa Baba Mtakatifu Francisko kwa serikali kuzingatia majukumu yao hasa kuhusiana na maswala ya uchumi wa kimataifa, unatokana na uhakika wake kwamba kuna jukumu la kisiasa katika kukabiliana na umaskini. Ila maandishi yake kabla ya kuchaguliwa kuwa Papa yanabainisha kwamba Francisko analiona hili kwani hapo 2011 (wakati uchumi wa Argentina ulipoanguka), Bergolio aliandika kwenye jarida la , kwamba “kuna waagentina wanaokumbwa na umaskini na kusukumwa pembezoni mwa jamii, ambao ni lazima tuwachukulie kama wadau na wahusika katika kuchonga hatima ya maisha yao wenyewe, na sio tu kama wafaidi wa misaada inayotolewa na serikali na mashirika ya kijamii”.

Lakini zaidi ya yote Francisko anawataka wakatoliki kuonyesha mwanga wa kikristo katika kukabiliana na swala la umaskini. Katika hotuba yake ya vigilia ya Pentekoste, alisisitiza kwamba lengo letu la kwanza lisiwe nguvu tendaji na kufanikiwa. “Ni kitu kimoja kumhubiri Yesu,” Francisko aliwaambia wasikilizaji wake, “na kitu kingine kufanikiwa.”

Haimaanishi kwamba wakristo hawana wajibu wa kufikiri na hata kujadiliana jinsi ya kuukomesha au kuupunguza umaskini. Ndivyo inavyodai haki. Francisko anataka kutuonyesha kwamba ikiwa tutashughulikia tu “mafanikio kwa mtazamo wa kidunia”, kuna hatari ya kuusahau upendo wa Kikristo.

Katika kuendeleza mjadala wake, Papa Francisko aliwauliza maswali mawili wale waliokuwa wakimsikiliza: “Niambieni, unapomsaidia mtu aneyeomba njiani, unamwangalia machoni baba au mama huyo?. . . Na unapomsaidia, unamshika mkono unayemsaidia au unamrushia tu vishilingi?”
Mambo matatu—kama asemavyo Francisko!—yanajitokeza hapa. Moja ikiwa ni: mara ngapi sote tumeanguka mtihani huu?

Pili ni Mwenyeheri Theresa of Calcutta. Hakuwa na mawazo ya kufanikiwa alipoamua kuwahudumia walio hoi zaidi miongoni mwa watu wa dunia. Katika maisha yake, alikaripiwa kwa kutokujihusisha zaidi kisiasa kuhusu baa la umaskini. Ila kazi yake haikuwa ya kisiasa. Ilikuwa juu ya kitu ambacho ni kikuu kuliko siasa: kuuleta upendo wa Kristo kwa wale ambao Kristo mwenyewe alituambia tutauona uso wake ndani mwao.

Na tatu ni kile ambacho Papa mstaafu Benedicto XVI alisisitizia sana kwenye waraka wake wa kwanza wa kipapa, , Mungu ni Upendo. Ijapokuwa waraka huu ulisisitiza sana maswala ya haki, Benedict wa kumi na sita alikazia kwamba kuna kitu ambacho kila mtu anayekumbwa na mateso anakihitaji zaidi: “upendo wa kipekee na kuthaminiwa.”

Kwao Baba Mtakatifu Francisko, mtangulizi wake (Benedikto wa kumi na sita), na Mwenye heri Mama Theresa (Wa Calkutta), jibu letu kuhusiana na umaskini lazima liwe, juu ya yote, kuonyesha haswa huruma, ambayo ndiyo kiini cha Injili. Pamoja na mambo mengine, hii inasaidia kusahihisha ule mwelekeo wa kibinadamu kwamba haki tu inatosha. Mungu angekuwa ni Haki tu, bila Upendo asingeweza kushuka na kuingia kwenye historia ya wanadamu kwa umbo la Yesu Kristo ili kutuokoa kutokana na sisi wenyewe. Tulikuwa hatumdai Mungu chochote. Kwa maana hiyo, basi, uelewa wa Kikatoliki kuhusu umaskini unatukumbusha kwamba ni Huruma ya Kimungu, na sio haki, ambayo inatuokoa.
Imehaririwa na Sista Brigita Samba Mwavasi








All the contents on this site are copyrighted ©.