2013-10-12 16:18:08

Sanamu ya Mama Yetu wa Fatima yawasili Rome.


Kwa ajili ya maadhimisho ya Siku ya Bikira Maria -Roma, Jumapili 13 Oktoba 2013, Papa Francisco ataongoza Ibada ya Misa ya Ekaristi kwa nia ya kuomba ulinzi na maombezi ya Mama Maria Mtakatifu Sana wa Fatima , kwa ajili ya kanisa la ulimwengu na dunia kwa ujumla .

Kwa ajili hii Sanamu asilia ya Mama Yetu wa Fatima, imeletwa kwa mara ingine Roma, pia kama sehemu ya maadhimisho ya matukio ya Jimbo la Roma kwa Mwaka wa Imani .

Sanamu ya Mama Yetu wa Fatima , inawasili Jumamosi hii jioni tokea Fatima, na itapokelewa Vatican Papa Francis wakiwepo pia Askofu Mkuu Rino Fisichella , Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza Uinjilishaji Mpya. Na pia waamini na maelfu ya waamini na mahujaji waliofika katika uwanja wa kanisa kuu la Mtakatifu Petro kutoa heshima zao kwa Mama Yetu wa Fatima.

Sanamu ya Mama Yetu Fatima mara ya mwisho, iliondoka katika makazi yake Fatima Ureno, wakati wa Maadhimisho ya Jubilee Kuu ya miaka elfu mbili ya Ukristu, kwa agizo la Mwenye Heri Yohane Paulo 11, tarehe 13 Mei kama ishara ya kuweka maisha yake yote chini ya ulinzi wa Mama Maria.
Jumamosi akitoa maaelezo kwa waandishi wa habari, Askofu Mkuu Rino Fisichella, alikumbuka mapenzi makubwa aliyokuwa nayo MwenyeHeri Karol Wojtyla,kwa Mama Yetu wa Fatima, ambaye alipenda tarehe siku aliyopigwa risasi na kujeruhiwa hapo Mei 13 , 1981, aweke taji kwa Sanamu ya Mama Yetu wa Fatima, aliye watokea watoto watatu wa Fatima Ureno. Mwenye heri Yohane Paulo 11 , aliamini ni Mama Yetu wa Fatima, ndiye aliyemwokoa na shambulio hilo. Na hivyo alijiweka chini ya ulinzi wa Mama yetu wa Fatima, kama mlinzi na mwombezi wake. Katika maisha yake yote. .
Na kwamba katika muda wa siku hizi mbili, Sanamu ya Mama Yetu wa Fatima, ikiwa Roma na Vatican, kama kawaida, waamini watafanya hija katika Kaburi la Mtakatifu Petro , na kusikiliza Katekesi ya Papa atakayoitoa katika Uwanja Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro .

Baada ya kuwasili Vatican, kutoka Fiumicino , sanamu ya Mama yetu wa Fatima, itapelekwa katika kanisa dogo la Monesteri anakoishi Papa Mstaafu Benedict XVI, ambako atafanya sala binafsi kwa muda mfupi. Na baadaye Sanamu itapelekwa katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta ambako itapokelewa na Papa Francisko. Na baadaaye sanamu itapelekwa kwa Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, ikiwa imebebwa na waumini wa kujitolea , chini ya ulinzi na usimamizi wa jeshi la “The Swiss guards” na polisi wa na polisi Vatican. Na kisha sanamu itapelekwa katika madhabahu ya Maria ya Upendo wa Mungu yaliyoko nje kidogo ya jiji Roma,”Divino Amore” ambako kutakuwa na Ibada ya Rozare Takatifu na mkesha wa maombi na sala . Jumapili sanamu inarudi katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kwa ajili ya Ibada ya Misa ya Ekaristi itakayoongozwa na Papa, kwa nia ya kulikabidhi Kanisa katika ulinzi na maombezi ya Maria







All the contents on this site are copyrighted ©.