2013-10-11 15:27:35

Maoni ya Askofu Mkuu Michael Fitzgerald juu ya Hati ya Kichungaji ya amani duniani.


(Vatican Radio)Katika Waraka wa Kitume wa Papa Yohane XXIII, juu ya Amani Duniani(Pacem in Terris) mna kanuni muhimu ya uhuru wa dini, ukionyesha umuhimu wa mwendelezo wa mahusiano kwenye mchanganyiko wa dini leo hii.
Hayo ni maoni ya Askofu Mkuu Michael Fitzgerald , aliyekuwa Mjumbe wa Papa Misri na Rais wa zamani wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mazungumzano kati ya Dini.

Askofu Mkuu Fitzgerald, alitoa maoni hayo wakati akizungumza na Philipa Hitchen wa Radio Vatican , wakati akiwa Roma kuhudhuria mkutano wa hivi karibuni, kwa ajili ya kuadhimisha miaka 50 ya barua ya Papa Yohana XXIII , Pacem in Terris.

Katika mahojiano, Philippa Hitchen alitaka kujua iwapo hati ya Papa Yohane XXIII aliyoiandika wakati wa vita baridi, inaweza kusaidia wale wanaofanya kazi ya kukomesha madhulumu ya kidini duniani kote leo hii. Na Askofu Mkuu Fitzgerald, kwanza alionya kwamba, hati hiyo haitoi hukumu kwa madhulumu yaliyokuwa yakifanyika dhidi ya Wakristu, lakini inatazama zaidi hoja ya matendo mema kama msaada katika kufanikisha mema kwa wote.

Na kwamba, kuna kanuni ya uhuru wa dini, hasa katika utendaji wa dini wa mtu , katika maisha yake ya kila siku, si tu katika maisha ya binafsi au umma kwa ujumla lakini pia katika , na uhuru wa dhamiri na imani ili kwamba mtu anaweza kubadili dini yake kama dhamiri yake inavyomtuma, jambo linaloleta matatizo hasa katika ulimwengu nchi nyingi za Kiislamu . Aidha kuna sheria potofu zinazo zuia ujenzi wa maeneo ya ibada kama makanisa au misikiti au watu kushiriki katika ibada mahali popote. Askofu Mkuu Michael anasema , huko ni kuwa kinyume na misingi ya haki za binadamu.
Katika vikwazo hivyo, inabidi kutafuta jawabu kupitia njia ya mazungumzano, hasa yanayolenga katika kuelewa maana ya haki za binadamu na kutekelezwa inavyopaswa.
Askofu Mkuu Fitzgerald, alieleza na kuonyesha kufurahia kwamba, kumekuwa na ishara nzuri za kutia moyo .... kama hatua iliyochukuliwa na Taasisi maarufu ya dini ya Kiislamu la Misiri Al-Azhar , kuruhusu masheikh na maimamu kushiriki katika mkutano wa Roma, ambako kwa pamoja wameweza kuuona mtazamo wazi wa mwelekeo wa dini nyingine, hivyo hiii imekuwa ni fursa ya kutafsiri katika hatua za kawaida na msaada wa kupanua uelewa kwa Waislamu na kwa Wakristo pia kuona hakuna sababu za kushambuliana kwa sababu za kidini. Bali dini inapaswa kuwa chombo cha kukuza amani na maelewano.








All the contents on this site are copyrighted ©.