Mkutano waandaliwa juu ya watu na misingi ya maisha ya kijamii
Baraza la Kipapa kwa ajili ya Familia , katika maadhimisho ya kutimia miaka 30, tangu
kutolewa kwa Hati ya haki za Familia , Baraza limeandaa Mkutano utakaoongozwa na Mada:
Mwelekeo mpya wa kijamii na haki za Familia . Mkutano huo utafanyika hapo 24 Octoba
mjini Roma katika jengo la Domus Pacis.
Kwa ajili hiyo , Baraza la Kipapa kwa ajili ya
Familia , linawaalika wote wanaopenda kuwa mtazamaji katika mkutano huu, kutuma
barua pepe kwa: . barua zitapokelewa hadi Ijumaa 18 Octoba 2013.