Miaka kumi tangu kutangazwa Mtakatifu Daniel Comboni
Wakati Mama Kanisa anapoadhimisha miaka kumi tangu kutangazwa mtakatifu Daniel Comboni,
shirika la Wamissionari wa Comboni wa Moyo wa Yesu wanasema wanayo sababu ya kuyasheherekea
maisha ya Mtakatifu huyu ambaye aliweka jiwe la msingi la maisha yao ya kimissionari.
Kwenye
makala yaliyoandikwa na Mkuu wa shirika hilo, Padre Enrique Sanchez Gonzalves, na
kuchapishwa na gazeti la Kila siku la Osservatore Romani la Roma, shirika hilo linasema
ni wakati muafaka wa kuadhimisha kwa furaha utakatifu wa mtu aliyeyatoa maisha yake
bila ya kujibakiza kwa ajili utume wa kimissionari. Daniel Comboni aliufungua moyo
wake na kumwachia Mungu kuuongoza alipopenda yeye Mungu, na hivyo kuweza kutwaliwa
kwenye nchi geni ambapo aliishi na kutoa huduma ya kitume hadi mwisho wamaisha yake.
Anasema Padre Enrique kwamba Comboni aliupokea mpango wa Mungu na kuwa mwaminifu,
katika kuufuata na kuisoma hadithi ya mwanadamu akitumia macho ya Mungu. Uaminifu
huo ndio ulioelekea kuchipuka kwa familia ya Wakomboni ambao hata leo wanaendelea
kujitolea kidete kwa ajili ya wokovu wao na wa ndugu zao sehemu mbalimbali duniani.
Kwa ajili ya majitoleo ya Comboni, anasema Padre Generali wa shirika la WaComboniani,
Wanachama wake wamefahamu kwamba utakatifu unawezekana ikiwa kuna mshikamano wa nia,
na kujibiidisha kwa pamoja kwa ajili ya wana wapenzi wa Mungu wanaokumbwa na changamoto
mbalimbali na wenye kusukumizwa pembezoni mwa jamii.
Anasema pia kwamba utakatifu
unawezekana pale penye unyenyekevu na unyofu katika kuendeleza mshikamano na dunia
yenye kuyajali maslahi na haki za wanyonge, na hata kwa kukubali kuhudumu kwenye maeneo
ambayo wengi wasingependa kufanya kazi.
Ni wakati pia wa kuukumbatia msalaba
huku wakitambua kwamba mbegu za utakatifu pia hukua chini ya msalaba, na kwamba maisha
ya mmissionari sio ya kutafuta faida yake mwenyewe au starehe, hadhi, ustawi na raha
maishani, vitu ambavyo vinazidi kupewa kipaumbele licha ya mateso mengi yanayowakumba
wengi wanaosahaulika na jamii. Ila maisha ya umissionari humhitaji mhusika kutopenda
kupewa heshima au kutafuta maslahi yake mwenyewe, na badala yake, kama alivyofanya
Mtakatifu Comboni, kuwa tayari kutumiwa na Mungu kwenye mpango wake wa kuwaongoa watu
wake.
Kuukumbatia utakatifu wa Comboni kunamaanisha kukubali kutemebea kwenye
njia ya msalaba kujitoa sadaka, kusali, na kufuata mantiki ya Mungu na sio ile ya
binadamu. Ni kupokea kwa unyenyekevu neema na huduma ya utakatifuzaji na kumwachia
Kristokuyatawala maisha, anasema Padre Enrique.
Padre huyu pia amemshukuru
Baba Mtakatifu Francisko kwa kuwachangamotisha maaskofu, Mapadre na wote wenye kuhudumu
ndani ya Kanisa kuwa wachungaji wema wenye kuitambua harufu ya kondoo wao, ambayo
pia ndiyo harufu ya utakatifu wao.