JImbo la Kondoa nchini Tanzania, linajiandaa kuliweka wakfu Kanisa Kuu la jimbo wakati
wa maadhimisho ya sikukuu ya Mtakatifu Paulo wa Msalaba, hapo tarehe 19 mwezi October,
2014.
Akiongea hivi karibuni na mtandao wa habari wa Baraza la Mabaraza ya
Maaskofu Afrika mashariki nay a kati, AMECEA, Askofu Bernardini Mfumbusa wa jimbo
la Kondoa amesema kwamba jimbo liko kwenye harakati za mwishomwisho katika ujenzi
wa Kanisa hilo kuu la Roho Mtakatifu, na kwamba hapo mwakani litakuwa tayari kuzinduliwa
kirasmi.
Jimbo la kondoa lilianzishwa mnamo mwaka 2011, na lilimegwa
kutoka jimbo la Dodoma.
Askofu Mfumbusa anawashukuru wote waliofanikisha
ujenzi wa kanisa hilo, huku akisema majimbo mengine kama vile Arusha Dodoma na Dar
– es – Salaam yalichangia kiasi kikubwa kwenye ujenzi huo. Amewashukuru waumini wa
majimbo hayo, wakiwa ni walei, watawa na mapadre waliojitolea kidete kuona kwamba
jimbo lina Kanisa Kuu.
Pia ameyashukuru mashirika yaliyochangia kwenye ujenzi
wa kanisa hilo kama vile Propagada Fide, (Vatican), Missio-Munich, (Germany); Baraza
la Maaskofu Katoliki Marekani, (USCCB) Solidarity Fund for Africa, Kirche in Not,
Wamissionary wa Mtakatifu Peter Clavery, na Jimbo la Bolzano-Bressanone (Italy).
Jimbo
la Kondoa lina waumini WasioMpaka kumalizika, Kanisa kuu la Roho Mtakatifu la Kondoa
litakuwa limetumia Tsh. 816,000,000 (sawa na Euro 388,571.) Kondoa ndilo jimbo dogo
zaidi Tanzania, likiwa na waumini wa kikatoliki 50,000 kati ya wakaaji 450,000 wa
wilaya hiyo.