2013-10-04 14:24:03

Siku ya Kimataifa ya kupinga vurugu,ukatili na mapigano


Jumatano, Oktoba 2, kwenye Umoja wa Mataifa, kuliadhimishwa Siku ya Kimataifa ya kupinga vurugu na ukatili. Siku hii pia, India huadhimisha kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa Mahatma Gandhi, mtu mashuhuri wa India , aliye eneza ujumbe wa kupigania haki na uhuru bila vurugu au ghasia. Hafla Kkatika Umoja wa Mataifa iliandaliwa na ubalozi wa India kwenye Umoja wa Mataifa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon, akiwa mgeni rasmi, alitoa wito kwa watu wote duniani, wakubali kuongozwa na roho wa kupenda wengine na kuikataa roho katili ya kudhuru wengine. Ban Ki Moon alitoa rai hiyo, akitazamisha katika ushupavu na ujasiri wa Mahatma Ghandi, mtu mashuhuri katika wajibu wa kutafuta haki kwa njia ya amani na kuvumiliana. .
Tarehe 2 Octoba ,kila mwaka ilitengwa na Baraza Kuu la umoja wa Mataifa kwa ajili ya kueneza ujumbe wa amani, kupitia elimu na ufahamu kwa umma.
Balozi wa kudumu katika umoja wa Mataifa toka India, Asoke Kumar Mukerji, alitoa ujumbe wake kwamba, “mazungumzo na uelewano wa kutoandama vurugu umejitokeza kuwa chombo muhimu cha kisera, iwe ni katika kutatua mizozo ya silaha au kutoa mkakati wa ukuaji na maendeleo, ni ulimbo unaowaunganisha wanadamu, licha ya tofauti zao nyingi.
Alisisitiza njia hii ya majadiliano bila vurugu na kupingana, si tu inahusu kuubadili ulimwengu, bali pia kumbadili mtu binafsi. Na Mahatma Gandhi daima alikumbusha kuwa majadiliano na mazungumzano katika hali ya amani na utulivu , ni ndiyo njia ya watu jasiri, na wasio waoga. Hivyo ametaja kwamba ni jukumu kupinga vurugu na ukatili, ili kusaidia kuweka dunia yenye amani kwa wote."
Wawakilishi wa nchi mbali mbali walitoa hotuba za kumuenzi Mahatma Gandhi na wengine kama Martin Luther King Jr na Nelson Mandela, na kusisitiza haja ya kuepuka vurugu,ila kujenga tabia ya kuvumiliana na kuendeleza mazungumzo ya amani.







All the contents on this site are copyrighted ©.