Buea Mwenyeji wa kilele cha Maadhimisho ya Mwaka wa Imani - Cameroon
Jimbo la Bueu limeteuliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Cameroon, kuwa mwenyeji wa
Maadhimisho ya Kitaifa ya kufunga mwaka wa imani. Shamra shamra za maadhimisho haya
zimeanza Alhamis Octoba 3, 2013, na inategemewa zaidi ya mahujaji elfu sita kutoka
pande mbalimbali za Cameroon wakiongozwa na Maaskofu wao 33 watashiriki katika kilele
cha maadhmisho haya.
Kwa ajili hiyo, Tume ya Maandalizi ya sherehe hizi, imetenga
mahali maalum katika Kanisa Kuu la Katoliki la Small Soppo, kwa shamrashamra hizi.
Inakumbukwa tarehe 21 Septemba 2013, Askofu wa Bueu alikutana na wanahabari na umma
kwa ujumla kueleza nini maana ya sherehe hizi za Kanisa. Na alisema, Imani ni zawadi
kutoka kwa Mungu , na kupitia Imani, waumini huungana na Mungu.
Na kwamba
, Yesu Kristu aliitoa zawadi hii kwa binadamu bure ya kuwa pamoja na Mungu. Lakini
pale imani inapokosa , binadamu huvunja uhusiano wake na Mungu. Na ndiyo maana kanisa
linatoa wito kwa watu wote kuishi na imani kwa Kristu, ili wawe katika umoja kamili
na Mungu. Basi Mwaka wa Imani, Askofu Bushu aliendelea kusema, ulilenga kuamsha upya
imani kwa Kristu, hasa ambao waliokuwa wamejiweka mbali na Mungu kutokana na mabadiliko
ya kidunia. Mambo mengi sasa yanafanyika na kututenga na Mungu. Tunamezwa na mambo
ya kidunia lakini sasa tumesema basi yatosha .
Hivyo sherehe hizi za kuufunga
Mwaka wa Imani, zinafungua kipindi kipya cha imani thabiti kwa Kristu, hasa katika
kupambana na changamoto zote zinazotaka kumtenganisha na Mungu , alisisitiza Askofu
wa Buea.
Shughuli za Kilele cha kuufunga mwaka wa Imani , zinaongozwa na
Mjumbe wa Kitume wa Papa nchini Cameroon, Askofu Mkuu Piero Pioppo. Kati ya matukio
yatakayofanyika ni pamoja na uwepo wa warsha , semina na makongamano yanayolenga
kuwa na hoja za kuimarisha imani ya Kikristu. Na kai ya wageni waalikwa ni pamoja
na Mratibu wa kanisa la Presbyterian Cameroon, naKatibu Mkuu wa Kanisa la Baptist
Cameroon.