2013-09-27 15:46:23

Mkutano wa OASIS juu ya Katiba- Zambia


Mshikamano wa Makanisa na mashirika ya kijamii nchini Zambia (OASIS Forum), unaiomba serikali ya Zambia kuwaruhusu wananchi wake kuchunguza mswada wa katiba kabla haujawasilishwa bungeni na kupitishwa kama sheria kuu ya nchi hiyo. Hii itakuwa ni fursa kwa wana Zambia kuhakikisha kwamba maoni yao yametiliwa maanani katika kurekebisha katioba ya nchi hiyo.

Haya ni kwa mujibu wa ujumbe wa Oasis Forum kwenye vyombo vyahabari vya nchi hiyo, siku ya jumanne (24/09/2013). Ujumbe huo uliotiwa sahahi na Padre Cleophas Lungu ambaye pia ni Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Zambia umetoa mwito kwa uongozi wa serikali, wana kamati ya Katiba, na Waziri wa Haki wa Zambia kuonyesha uzalendo wao na kuyafuata maadili ya katiba kuhusiano na utaratibu huo.

OASIS Forum pia inasisitiza kuwepo kwa kipengele chenye kulinda utaratibu wa kutengeneza Katiba, kwenye sheria za nchi hiyo. Ukosefu wa kipengele hicho, unasema ujumbe wa OASIS Forum, unasababisha kutozingatiwa kwa taratibu na maadili yenye kuongoza shughuli hiyo ya urabati wa sheria kuu ya nchi hiyo.

OASIS Forum ni kundi ambalo linayashirikisha makundi ya kiimani na yale yenye kutetea haki jamii nchini Zambia. Wanachama wa OASIS Forum ni pamojana Baraza la Makanisa, Zambia CCZ; Usharika wa Kiinjili Zambia, EFZ); Baraza la Maaskofu Katoliki, Zambia, ZEC; Kamati kuu ya Mashirika yasiyo ya kiserikali, NGOCC; na Umoja wa Wanasheria wa Zambia, LAZ.

OASIS Forum wamekuwa mstari wa mbele katika kutetea utengenezaji wa katiba mpya nchini Zambia na kuhakikisha kwamba shughuli hiyo inafanyika kwa njia wazi kabisa kwa manufaa ya wananchi wote wa Zambia. Mshikamano huo pia umekuwa ukiwashauri wa Zambia kuungana kidete kwenye zoezi hilo la kitaifa na kuhakikisha kwamba linafikia kikomo chake kwa amani.








All the contents on this site are copyrighted ©.