2013-09-25 15:01:18

Umoja wa Kanisa ni zawadi toka kwa Mungu .


Baba Mtakatifu Francisko, katika Katekesi yake kwa mahujaji na wageni, ameendelea kuitafakari sala ya Nasadiki akisema, ndugu zangu wapendwa, katika sala ya Nasadiki tunakiri kwamba Kanisa ni moja. Na tunapofikiri wingi wa utajiri wa lugha na utamaduni wa watu waliomo katika Kanisa duniani kote , tunapata kuelewa zaidi kwamba umoja huu wa kanisa ni zawadi toka kwa Mungu.Zawadi ambayo chimbuko lake ni ubatizo mmoja na katika kushirkishana imani moja ya kanisa na maisha ya kisakramenti. Na Kanisa kama familia kubwa , tumeungana wake kwa waume , wote pamoja katika Kristo, popote pale tulipo

Papa aliendelea kusema, tunaweza kujiuliza ni kiasi gani sisi kama Wakristu tunafurahia na kueleza na maisha yetu ya kila siku kushuhudia hayo, na hasa katika maombi yetu, ukweli huu wa umoja na mshikamano wetu, katika usharika wa Kanisa.
Papa amehimiza Wakristu kutambua kwamba, dunia inahitaji shuhuda za kimaisha kuonyesha mpango huu wa Mungu , katika mapatano, usharika, na amani ya familia nzima ya binadamu.

Papa alieleza na kuhitimisha maelezo yake kwa kumwomba Bwana, awawezeshe Wakristo wote duniani, kufanyakazi kwa ajili ya kuishinda mivutano na migawanyiko iliyopo kati ya Wakristu, na wadumu katika umoja , kama alivyosema Mtakatifu Paulo, “ kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. Mwili mmoja na Roho mmoja kama mlivyoitwa katika tumiani moja la wito wenu. na kufurahia mapatano kwa roho anayetengeneza utajiri wa wingi wenu mlio tofauti. taz. Efe 4:03








All the contents on this site are copyrighted ©.