2013-09-25 08:18:52

cheni mapigano, na kuzingatia mazungumzo, nchi za maziwa makuu


Umoja wa mataifa unasema kwamba nchi zinazopakana naJamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Congo zimekubali kutoingilia kati maslahi ya ndani ya nchi jirani zao kama njia moja ya kutekeleza mkataba wa amani ulioafikiwa na nchi zilizomo kwenye maeneo ya maziwa makuu mapema mwaka 2013.

Haya yamesemwa na Bi Mary Robinson, Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye eneo la Maziwa Makuu siku ya jumatatu kwenye kikao na wawakilishi kutoka mataifa kumi ya eneo hilo, na wawakilishi wa kanda mbili za bara Afrika. Amesema mjumbe huyo kwamba kazi iliyobaki ni kuhakikisha kwamba uamuzi huo unatiliwa maanani na kutimizwa na kila nchi mwanachama wa maeneo hayo.

Migogoro ya kivita inayoendelea hivi sasa nchini Congo ni kati ya wanamgambo wa M23 na majeshi ya DRC. Ripoti kadhaa za uchunguzi wa Umoja wa Mataifa zinabainisha kwamba nchi ya Rwanda imekuwa ikilisaidia kundi la waasi la M23 na kutumia fursa hiyo ili kuingia nchini DRC na kujifaidisha na biashara ya madini kwenye eneo la mashariki la nchi ya DRC.

Naye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban ki Moon ambaye amefanya mkutano na mwenyekiti wa Kamati ya Umoja wa Afrika, Nkosazana Dlamini – Zuma, ameshtumu vitendo vya kundi la M23 na makundi mengine ya wapiganaji wanaoendelea kusababisha mateso mengi kwa wenyeji wa mashariki mwa DRC.

Bi. Robinson ameutaja mkutano huo kuwa na mafanikio makubwa huku akisema baada ya mkutano huo aliwaona marais Paul Kagame wa Rwanda na Joseph Kabila wa Congo wakiongea pamoja kwa namna ya kirafiki.











All the contents on this site are copyrighted ©.