2013-09-19 14:52:06

Sista Angèlique ,mtawa wa Congo, ashinda tuzo ya Nansen2013.


Mtawa Sista Angèlique Namaika, Mkatoliki ambaye amekuwa kwa muda mrefu akisadia wanawake wanaodhulumiwa kijinsia na Maaskari na waasi wa kikundi cha maasi cha LRA, katika Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo , DRC, ametajwa kuwa kuwa mshindi wa tuzo ya Umoja wa Mataifa ya Wakimbizi, kama kutambua juhudi zake, katika kusaidia wakimbizi.

Sista Angelique Namaika, amesaidia zaidi ya wanawake na wasichana 2,000 waliodhulumiwa kinjisia na waasi wa LRA, katika kipindi cha muongo mmoja uliopita. Sista huyo anayejulikana kwa wakimbizi wengi DRC, atapokea tuzo ya Nansen mwishoni mwa mwezi huu.

Tuzo ya Wakimbizi ya Nansen, hutolewa kila mwaka na shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa kwa waliotenda zaidi katika mazingira ya wakimbizi , na kwa mwaka huu, unhcr, imetambua utendaji usiokuwa wa kawaida wa Sista Angelique, ambaye ameanzisha kituo katika mji wa Dungu, Kaskazini Mashariki wma DRC, cha kutoa msaada kwa wanawake na waichana wanaodhulumika kijinsia.

Kituo cha Dungu , kimeweza kubadili maisha ya wanawake wingi , kwa kutoa elimu na mafunzo msingi katiak maisha yao . Tuzo ya Nansen, imetajwa kwa heshima ya Fridtjof Nansen, mgunduzi mashuhuri , Mwanasayanasi na Mwanasiasa aliyekuwa Kamishena wa kwanza wa Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa. Sista Angelique atapokea tuzo yake Septemba 30, mjini Geneva. Na Octoba 2 , atakuwa Roma ambako atakutana na Papa Francisko.








All the contents on this site are copyrighted ©.