Askofu Shao asema, hali ya Padre Anselmo bado ni mbaya.
Askofu Augustine Shao, wa Jimbo Katoliki Zanzibar, Jumanne (18 Septemba 2013), aliieleza
hali ya Padre Anselmo Mwanagamba kuwa bado ni mbaya, kutokana na tindikali aliyomwangiwa,
kupenya hadi chini ya ngozi. Na hivyo wanatazama uwezekano wa kumpeleka katika hospitali
zenye utalaam zaidi, ikiwezekana nje kama India, ambako kuna uzoefu wa kutosha kwa
matatizo kama hayo.Hayo alieleza Jumanne katika mahojiano na shirika la habari la
Fides na kunukuliwa na CISA.
Padre Anselmo Mwanga'mba, Padre wa Kanisa Katoliki
Zanzibar, kwa wakati huu amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kitaifa ya Muhimbili,
ambako alihamishiwa tokea Hospitali ya Mnazi mmoja Zanzibar alikolazwa baada ya kumwagiwa
tindikali na watu wasiojulikana. Padre Anselmo alishambuliwa wakati akitoka katika
kituo cha Internet Ijumaa iliyopita.
Padre Anselmo ni mhanga wa mashambulio
mfululizo ya kutumia tindikali, yalitokea katika kisiwa cha Zanzibar katika miezi
ya karibuni. Waathirika wengine ni pamoja na mabinti wawili raia wa Uingereza, waliofika
Zanzibara kama walimu wa kujitolea, na pia Fadhil Suleiman , Katibu wa Mufti Mkuu
wa Zanzibar.
Askofu Shao anasema , Suala la mashambulizi haya ni tata, kwani
tangu mwaka jana, wameshuhudia matukio makubwa ya maonevu na dhuluma kwa Kanisa Katoliki
na Wakristu kwa ujumla Zanzibar. Askofu Shao, ameeleza kwa kukumbuka matukio mengine
ya Mapadre kushambuliwa, Padre Mkenda Ambrose alijeruhiwa vibaya wakati wa Siku Kuu
ya Krismasi mwaka jana, ambaye hali yake bado si nzuri , na Februari mwaka huu Padre
Evarist Mushi, aliuawa na watu wasiojulikana wakati akielekea kuadhimisha Ibada
ya Misa. .
Askofu Shao, ametaja sababu kadhaa za unyanyasaji huo kwamba ni
pamoja na mivutano ya kisiasa juu ya Katiba mpya na kuibuka kwa vikundi vinavyotaka
Zanzibar iwe nchi huru kamili, badala ya kushikamanishwa na Tanganyika, pia kuna
kutoelewana juu ya marekebisho ya orodha ya wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi 2015.
Na kwa mtazamo wa athari za kiuchumi kijamii, ipo hisia kwamba wageni toka bara
na mataifa mengine kama Kenya , wengi wao wakiwa Wakristu, wanapokonya nafasi za kazi
kwa Wazanzibar. Na hatimaye kuna Waislam wenye msimamo mkali, ambao hupigia debe
propaganda inayoenezwa kichinichini na wageni wenye kutoa mafunzo ya mahubiri ,
yenye kueneza chuki dhidi ya wakristo, hasa kwa vijana wa Kiislamu wa visiwani humo.
Vijana hao walipelekwa mafunzo nje ya nchi na sasa wanaigiza moyo na mawazo ya chuki
na fitina Zanzibar, kupitia mihadhara na vyombo vya habari mahalia..
Amesema,
kwa kifupi , sababu za matendo maovu ni nyingi. Na hali ni ngumu, lakini hana uhakika
kama Wakristu na hasa Wakatoliki ni walengwa au wanatumika tu kama chambo katika
sababu hizo. Mbali na kushambuliwa Mapadre, pia , makanisa 4 yameharibiwa vibaya,
amehitimisha Askofu Shao , na kunukuliwa na Fides siku ya Jumatano.
Kufuatia
tukio la Ijumaa, watu 15 wanasadia polisi kuupata mtandao wa watu wanaofanya vitendo
hivi viovu. Na kuna hisia kwamba , yao ni wanachama wa kikundi cha uhalifu cha Somalia
cha al Shabab,a mbacho ni tawi la al Qaeda, kikundi cha kighaidi cha kimataifa.