Kila mwaka ifikiapo tarehe 21 mwezi Septemba, Umoja wa Mataifa huadhimisha Siku ya
Amani Duniani. Nayo kamati ya Kiekumeni ya Makanisa Duniani imewaomba waumini wote
wa makanisa yake kuombea amani siku hiyo.
Baba Mtakatifu baada ya katekesi
yake siku ya jumatano kwa halaiki ya waumini na wahujaji waliokusanyika kwenye uwanja
wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatikani, amewaalika waumini wakatoliki kote
ulimwenguni kuungana na wakristo wenzao katika jitihada za kumwomba Mungu kuwajalia
zawadi ya amani wote wenye kuishi kwenye maeneo yanayokumbwa na migogoro ya kivita.
Ni ombi la Baba Mtakatifu Francisko kwamba amani itawale kwenye mioyo ya watu
wote, na kwamba kila mtu atajitahidi kuwashawishi viongozi wa dunia kutafuta suluhisho
la kidiplomasia na kisiasa kwa ajili ya kuleta amani kwenye maeneo ambayo wakazi wake
waanaendelea kuteseka kwa ajili ya migogoro.
Ni mazungumzo na majadiliano tu
yanayoweza kuleta amani ya kudumu na kuhakikisha kwamba haki na heshima ya kila mwanadamu,
na hasa wale walio dhaifu zaidi, inaendelezwa, asema baba Mtakatifu.