2013-09-18 08:06:34

Papa akutana na Mapadri wa Jimbo la Roma


Mapadre wa Roma wanampenda Mungu, wanaupenda utume wao na ni waaminifu katika kazi yao ya kichungaji huku wakipenda na kuwa karibu na wote wanao hitaji huduma zao. Haya yamesemwa na Cardinali Agostino Vallini, Vika wa Roma alipokuwa akimkaribisha Baba Mtakatifu Francisco kwenye jumuiya ya mapadre wa Roma wakati wa Mkutano na Papa siku ya Jumatatu kwenye kanisa Kuu la Mtakatifu Yohanne Laterano lililoko mjini Roma.

Alisema Mons. Valinni kwamba Mapadre wanatajirika na kupata nguvu mpya kwa maneno na matendo ya Khalifa wa Mtakatifu Petro, Papa Francisko tangu kuchaguliwa kushika wadhifa huo Mwezi Machi mwaka 2013.

Mons. Vallini ameutaja ukakamavu na unyenyekevu wa Baba Mtakatifu Franscisko pamoja na jitihada zake za kuwa karibu zaidi na maskini na wale wanaosukumizwa pembezoni mwa jamii kama mambo ya kutia moyo na ambayo yamegusa mioyo ya watu wengi. Mons. Vallini amesema kwamba Papa amekuwa ni alama ya nyakati ambayo Mungu ameupatia ulimwengu na ambayo Mapadre wanapaswa kuiona kama mwaliko wa kujirudi na kuyahuisha upya maisha yao na mwaliko wao wa kumfuasa kristo kwa karibu zaidi.

Naye baba Mtakatifu ameendelea kuwaasa wanae wapendwa mapadre akisema kwamba kanisa linao watakatifu wengi mbali na changamoto za hapa na pale, na kwamba utakatifu huo ndio wa kupewa kipaumbele cha kwanza, utakatifu wa kuish maisha ya kawaida kiaminifu kama wafanyavyo wamama na wanawake na wanaume watakatifu wengi sana duniani wanaoendeleza familia zao bila ya kujishaua. Ni utakatifu huo unaoliimarisha kanisa, anasema Papa, na kwamba sio kutenda mambo yasiyo ya kawaida au kuonyesha ujasiri mkuu kunakomfanya mtu kuwa mtakatifu, bali kuyaishi kiaminifu na kikamilifu maisha ya kila siku na changamoto zake zote.











All the contents on this site are copyrighted ©.