Tweet, Papa ashukuru wote walio shiriki mkesha wa sala ya kuombea amani.
Ujumbe wa Papa kwa siku ya Jumanne , kupitia ukurasa wa tweet @ pontifex, umetoa
shukurani za dhati kwa wote walio shiriki mkesha wa sala ana mafungo kwa ajili ya
kuombea amani Syria na duniani kote. Kama ilivyokuwa Jumapili, wakati wa Sala
ya Malaika wa Bwana, Papa ameendelea kutoa ombi lenye kuwataka watu wote wakazane
kuombea amani Syria , Mashariki na kati na duniani kote. Amesema vita pekee tunayopaswa
kupigana nayo kwa wakati huu , ni mapambano dhidi ya dhambi na maovu.