2013-09-11 15:49:22

Papa ahimiza wenyeji kuwa na ukarimu wa ziada kwa wageni wahamiaji na wakimbizi


Papa Francisko Jumanne jioni,(10.9.2013) alikitembea kituo cha wakimbizi cha Astalli hapa Roma kinachosimamiwa na shirika la Wajesuit kwa ajili ya wakimbizi (JRS). Akiwa mahali hapo aliuita wingi wa mchanganyiko watu wenye asili mbalimbali na dini mbalimbali kuwa ni utajiri unaopaswa kupokelea kwa mikono miwili, bila woga wala mashakamashaka.

Papa alisema kuna haja gani ya kuogopaogopa, iwapo imani ya kila mmoja ni thabiti? Ni nini hasa cha kuogopa? alihoji Papa. Papa aliutumia pia muda huo, kutoa shukurani zake za dhati kwa wafanyakazi na watu wa kujitolea kwa wema na ukarimu wao, katika majitoleo hay ya bila kujibakiza katika kuutumia pia muda mwingi kusaidia maelfu ya wakimbizi wanaopita katika milango ya kituo hicho kila mwaka , na kwa utambuzi wao kuwa hawa ni watu , na kufanyakazi kwa bidii kwa ajili ya kupata majawabu katika mahitaji yao.

Papa amelitaja jiji la Roma kuwa ni kituo cha pili kwa wakimbizi wengi wanaoingia Italy, kupitia mlango wa Lampedusa, wa Kusini mwa Italy. Na aiielezea safari yao watu hao tokea Afrika Kaskazini, kuwa ni ya kuchosha, zaidi ya yote ni watu wanao tafuta kuboresha hali yao ya maisha kwa ajili yao na watoto wao . Papa aliwaonea huruma zaidi wanawake na mama wengi wanaoanza safari hizi za kutafuta ahueni za maisha, kwa ajili yao na familia zao, bila ya kujali changamoto ngumu mbele yao.

Papa aliendelea kuonyesha kujali hali za wakimbizi na wahamiaji akihoji ni mara ngapi habari za madhulumu na kukosa msaada kwa watu hawa zimesikika , licha ya wengine kuwa hata hati halali ya ulinzi wa kimataifa au kuwa hati zinazo waruhusu kuishi katika Jiji la Roma, lakini bado watu hao wanalazimika kuishi katika mazingira mabovu na duni, ya kutisha , yenye kudharirisha utu wao na bila hata ya kupewa mwanya wa kufikiria juu ya hali yao ya baadaye!

Kwa hali hizo, Papa alipeleka mawazo yake kwa utume wa Wajesuit katika kituo cha Astalli, na kutoa pongeza kwamba, huduma yao ya kuwapokea na kuwakaribu wahitaji, wakiwa wamemezwa na roho ya msamaria Mwema na uelewa mpana , wanawainamia wenye shida na dhiki na kuwapa mkono wa karibu bila kuhesabu faida au kuwa na woga . Hii ni sehemu ya mshikamano, akilitaja neno mshikamano kwamba kwa wengine linaleta hofu hasa katika dunia iliyoendelea, uwepo wa woga, hata kulitamka, kama vile ni neno baya. Lakani kumbe ni neno linalopaswa kuwa kinywani mwa wote, Papa alisisitiza.
Kisha Papa alionyesha hamu yake kwamba, ziara yake hii katika kituo cha wakimbizi cha Astalli, na iitawweza kugusa mioyo ya wakazi wote wa Jimbo la Roma na kichocheo cha kutafakari jinsi wanavyoweza kutoa jibu kwa wito wa YesU Kristu, kuhudumia wahitaji , na bila ya kuukimbia uso wa mtu anayetafuta haki .
Na hii haimanishi tu kuwa mwema katika kutoa misaada kama chakula kwa mtu mhitaji, lakini pia ni kuwasaidia waweze kusimama tena, katika njia ya maisha ya kawaida yenye hadhi na heshima kamili. Papa alisisitiza huruma ya kweli , hudai haki, na Kanisa katika Jimbo la Roma na taasisi zake , linapaswa kuhakikisha hakuna yeyote katika Jiji hili anayekosa mlo wake wake wa kila siku au makazi au msaada wa kisheria katika kuzitambua haki zake za kuishi na kufanyakazi kama binadamu mwingine yoyote. Ni mshikamano wa kijamii unaodai utendaji wa haki kwa kila mtu.
Papa pia aligeukia nyumba za watawa watawa wa kike ambazo hazina tena watu , kwa ukarimu, kufungua milango kwa wakimbizi na kwamba Kanisa halihitaji nyumba hizo za watawa zisizokuwa na miito, kugeuzwa mahotel kama kitega uchumi cha kujipatia fedha. Hilo si lengo la Kanisa.








All the contents on this site are copyrighted ©.